WANAJESHI JWTZ WATUNUKIWA NISHANI ZA UMOJA WA MATAIFA SUDAN

WANAJESHI JWTZ WATUNUKIWA NISHANI ZA UMOJA WA MATAIFA SUDAN - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa WANAJESHI JWTZ WATUNUKIWA NISHANI ZA UMOJA WA MATAIFA SUDAN, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : WANAJESHI JWTZ WATUNUKIWA NISHANI ZA UMOJA WA MATAIFA SUDAN
kiungo : WANAJESHI JWTZ WATUNUKIWA NISHANI ZA UMOJA WA MATAIFA SUDAN

soma pia


WANAJESHI JWTZ WATUNUKIWA NISHANI ZA UMOJA WA MATAIFA SUDAN

​Na Luteni Selemani Semunyu
Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Kikosi cha 11 wametakiwa kujivunia mafanikio yaliyopatikana kufuatia  utumishi wao uliotukuka kwa kipindi cha Mwaka Mmoja waliokuwa wakishiriki Ulinzi wa amani Jimboni Darfur nchini Sudan na kutunukiwa Nishani ya umoja wa Mataifa.

Hayo yalibainishwa na mkuu wa majeshi ya Ulinzi ya umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa UNAMID   jimboni Darfur Luteni Jenerali Leonard Ngondi wakati wa sherehe za kuwatunuku Nishani Askari wa JWTZ  katika sherrehe zilizofanyika Khor Abeche na kuhudhuruliwa na Viongozi mbalimbali wakiwemo wa Serkali ya Sudan.

“ Kutunukiwa nishani ni jambo la Kujivunia kwa kuwa zimetolewa kwa sababu Askari wamefanya kazi Nzuri amabayo inapaswa kupongezwa hasa kutokana na Doria zilizofanyika ikiwemo katika safu za Milima ya jaber ambayo inakaliwa na Waasi” Alisema Luteni Jenerali Ngondi.

Kwa Upande wake Mkuu wa Operesheni ya Jaber Mara  Lameck Kawiche alitoa wito kwa Wanajeshi wa Tanzania kuendeleza utayari  wao ili kuhakikisha  wanalinda heshima ya jeshi hilo kwa kufanya kazi kwa Weledi ili kuepusha madhara yanayoweza kutokea kama ilivyotokea Nchini Kongo.

“ Najivunia Utimamu wa jeshi la Tanzania tuna kila sababu kumpongeza Rais na Amiri Jeshi kwa kuridhia Majeshi ya tanznia Kushiki Operesheni za Umoja wa Mataifa sambamba na Mkuu wa Majeshi kya Ulinzi kwa mafunzo kwa Wanajeshi Wake” Alisema  Kawiche.
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi UNAMID Jimboni Darfur Sudan, Luteni Jenerali  Leonard Ngondi ( wa Tatu  kushoto) akiwasili katika Uwanja wa ndege wa Khor Abeche katika sherehe za uvishaji nishani  walinda Amani kutoka Tanzania  Hivi karibuni wa nne Kushoto ni kamanda wa kikosi cha Tanzania Kanali Wiliam Sandy .(Picha na Luteni Selemani Semunyu.
Kamanda Kikosi cha Tanzania  TANZBATT 11 Jimboni Darfur nchini Sudan, Kanali William Sandy kulia akivishwa nishani na  Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi UNAMID. Luteni Jenerali  Leonard Ngondi katika sherehe za uvishaji nishani  walinda Amani kutoka Tanzania  Hivi karibuni.(Picha na Luteni Selemani Semunyu)
Mnadhimu Mkuu wa mpango wa pamoja wa Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa UNAMID akivisha nishani walinda Amani kutoka Tannzaia katika sherehe za uvishaji nishani walinda Amani kutoka Tanzania hivi karibuni katika eneo la Khor Abeche(Picha na Luteni Selemani Semunyu).


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA 



Hivyo makala WANAJESHI JWTZ WATUNUKIWA NISHANI ZA UMOJA WA MATAIFA SUDAN

yaani makala yote WANAJESHI JWTZ WATUNUKIWA NISHANI ZA UMOJA WA MATAIFA SUDAN Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala WANAJESHI JWTZ WATUNUKIWA NISHANI ZA UMOJA WA MATAIFA SUDAN mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/04/wanajeshi-jwtz-watunukiwa-nishani-za.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "WANAJESHI JWTZ WATUNUKIWA NISHANI ZA UMOJA WA MATAIFA SUDAN"

Post a Comment