title : SERIKALI YAONGEZA MUDA WA KUNYONYESHA KWA WATUMISHI WA UMMA NA MASHIRIKA NA SEKTA BINAFSI
kiungo : SERIKALI YAONGEZA MUDA WA KUNYONYESHA KWA WATUMISHI WA UMMA NA MASHIRIKA NA SEKTA BINAFSI
SERIKALI YAONGEZA MUDA WA KUNYONYESHA KWA WATUMISHI WA UMMA NA MASHIRIKA NA SEKTA BINAFSI
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii .
SERIKALI imeongeza masaa ya unyonyeshaji kwa watoto kwa watumishi wa serikali, mashirika pamoja sekta binafsi ili kuwezesha watoto kuwa na afya bora inayotokana na maziwa ya mama.
Hayo ameyasema Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati akifungua Wiki ya Unyonyeshaji, amesema kuwa mama mzazi baada ya kumaliza miezi mitatu ataingia kazini 3:30 na kuondoka saa 7:30 katika kumuwezesha mama kunyonyesha mtoto bila kuingiliwa na majukumu ya kikazi.
Ummy amesema kuwa watendaji wa Umma na mashirika pamoja na taasisi lazima wafanye hivyo katika kutambua umuhimu wa mama mzazi kunyonyesha kwa muda uliowekwa kwa kipindi cha miezi sita.
Amesema kuwa ni gharama kubwa katika kuhudumia watoto walio na utapiamlo ambao unatokana moja ni kukosa maziwa ya mama kwa muda mrefu hivyo kuepuka ni njia rahisi ikiwemo kutengwa kwa masaa hayo.
Waziri Ummy amesema kuwa suala la lishe lazima liangaliwe kwa ukaribu na wadau wote katika kuweza kuwaondoa watoto katika utapiamlo ambao unafanya kudumaa kwa akili.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akipata maelezo juu masuala ya lishe kutoka kwa mtaalam wa lishe wa Taasisi ya Chakula lishe nchini (TFNC),Neema Joshua wakati maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji leo.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akizungumza wakati wa ufunguzi wa wiki ya unyonyeshaji na uzinduzi usambazaji taarifa kwa njia ya simu leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chakula na Lishe Nchini(TFNC), Joyceline Kaganda akizungumza juu ya mikakati ya lishe na umuhimu wa unonyeshaji leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Lishe nchini (Panita), Tumaini Mkindo akitoa salamu za mashirika yasio ya kiserikali yanavyofanya kazi katika sehemu ya lishe kwa kuwa miradi mbalimbali.
Hivyo makala SERIKALI YAONGEZA MUDA WA KUNYONYESHA KWA WATUMISHI WA UMMA NA MASHIRIKA NA SEKTA BINAFSI
yaani makala yote SERIKALI YAONGEZA MUDA WA KUNYONYESHA KWA WATUMISHI WA UMMA NA MASHIRIKA NA SEKTA BINAFSI Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala SERIKALI YAONGEZA MUDA WA KUNYONYESHA KWA WATUMISHI WA UMMA NA MASHIRIKA NA SEKTA BINAFSI mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/08/serikali-yaongeza-muda-wa-kunyonyesha.html
0 Response to "SERIKALI YAONGEZA MUDA WA KUNYONYESHA KWA WATUMISHI WA UMMA NA MASHIRIKA NA SEKTA BINAFSI"
Post a Comment