title : SIMBA KUELEKEA SAUZI KWA MAANDALIZI YA MSIMU MPYA WA LIGI
kiungo : SIMBA KUELEKEA SAUZI KWA MAANDALIZI YA MSIMU MPYA WA LIGI
SIMBA KUELEKEA SAUZI KWA MAANDALIZI YA MSIMU MPYA WA LIGI
Timu ya Soka ya klabu ya Simba kesho alfajiri, inatarajia kwenda nchini Afrika kusini, kwa ajili ya kuweka kambi ya maandalizi ya msimu mpya unaotarajiwa kuanza mapema mwezi ujao.
Kambi hiyo ya siku Ishirini itahusisha wachezaji wote waliosajiliwa kwenye klabu,kwa msimu huu wa ligi.
Kwa upande wa wachezaji waliopo kwenye Timu ya Taifa,wao wataungana na wenzao,mara baada ya mchezo wa marudiano baina Taifa Stars na Rwanda,utakaochezwa wiki ijayo kule Kigali.
Ikiwa huko nchini Afrika kusini, kikosi hicho pia kitapata fursa ya kucheza michezo kadhaa ya kujipima nguvu,kabla ya mchezo wake wa tarehe nane mwezi ujao(SIMBA DAY),Mechi ambayo klabu huitumia kutambulisha wachezaji wake na jezi mpya ya msimu,mchezo huo utapigwa hapa jijini Dar es salaam,kwenye uwanja wa Taifa.
Wakati huo huo klabu ya Simba inaungana na wanamichezo na watanzania wengine,kumpa pole Waziri wetu mwenye dhamana ya michezo nchini Dr Harrison Mwakyembe kwa kuondokewa na Mkewe bi Linnah Mwakyembe.
Tunamuomba Waziri Mwakyembe awe na subira yeye na familia yake katika kipindi hiki kigumu,na klabu itashiriki shughuli zote za msiba wa mama yetu Linnah.
IMETOLEWA NA
IDARA YA HABARI NA MAWASILIANO
SIMBA NGUVU MOJA
Hivyo makala SIMBA KUELEKEA SAUZI KWA MAANDALIZI YA MSIMU MPYA WA LIGI
yaani makala yote SIMBA KUELEKEA SAUZI KWA MAANDALIZI YA MSIMU MPYA WA LIGI Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala SIMBA KUELEKEA SAUZI KWA MAANDALIZI YA MSIMU MPYA WA LIGI mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/07/simba-kuelekea-sauzi-kwa-maandalizi-ya.html
0 Response to "SIMBA KUELEKEA SAUZI KWA MAANDALIZI YA MSIMU MPYA WA LIGI"
Post a Comment