UBUNGO WACHAMBUA BAJETI YAO YA FEDHA,WAJIPANGA KUBORESHA UTOAJI HUDUMA KWA JAMII

UBUNGO WACHAMBUA BAJETI YAO YA FEDHA,WAJIPANGA KUBORESHA UTOAJI HUDUMA KWA JAMII - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa UBUNGO WACHAMBUA BAJETI YAO YA FEDHA,WAJIPANGA KUBORESHA UTOAJI HUDUMA KWA JAMII, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : UBUNGO WACHAMBUA BAJETI YAO YA FEDHA,WAJIPANGA KUBORESHA UTOAJI HUDUMA KWA JAMII
kiungo : UBUNGO WACHAMBUA BAJETI YAO YA FEDHA,WAJIPANGA KUBORESHA UTOAJI HUDUMA KWA JAMII

soma pia


UBUNGO WACHAMBUA BAJETI YAO YA FEDHA,WAJIPANGA KUBORESHA UTOAJI HUDUMA KWA JAMII

Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

MEYA wa Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam Boniface Jacob  ametaja vipaumbele 11 vya halmashauri yai vilivyomo katika Bajeti ya fedha kwa mwaka 2019/2020 ambayo pamoja na mambo nengine imejikita kuboresha utoaji huduma kwa jamii kwa kuongeza fedha za kujengea Makao makuu ya Halmashauri kiasi cha Sh.millioni 700.

Pia bajeti hiyo inaonesha kuanza ujenzi wa kujenga Hospitali ya wilaya kwa kiasi cha sh.Millioni 250,pamoja na kutengwa fedha za kujenga machinjio ya kisasa kiasi cha sh.Millioni 250 pamoja fedha Sh.milioni 300 ambazo zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa Soko la Mbezi( kwa ajili ya wamachinga).

Akizungumza zaidi kuhusu makadirio ya fedha hizo za bajeti jana wilayani Ubungo jijini Dar es Salaam ,Meya Jacob amefanunua kuwa  Serikali itatoa ruzuku ya Sh.Billioni 65.5, Sh.Millioni 750 ni michango ya Wananchi na Sh.billioni 18.4 ni makusanyo ya ndani.

Pia amesema Sh.,Billioni 72.3 ni Mishahara ya watumishi na Sh.billioni 12.3 zimeelekezwa katika miradi Mbalimbali ya Maendeleo.Aidha ameweka msisitizo kuwa Kiasi cha Sh.billioni 8.3 sawa na asilimia 60,za mapato yanayokusanywa na Halmashauri zitatumika kwa ajili ya Miradi ya maendeleo.

Jacob amezungumzia pia uimarishwaji wa Utawala bora kwa kuwatengea fedha za kiinua Mgongo ,wenyeviti wa Serikali za mitaa wanaomaliza muda wao mwaka 2019

"Kuongeza Mapato kwa kuboresha miundombinu ya ukusanyaji,kubuni vyanzo vipya,Uanzishaji wa stendi za daladala Mloganzila na Msumi,Uanzishwaji wa Masoko mapya Kiasi cha Sh.Billioni 1.7 zimetengwa

" Tumedhamiria kuongeza kiwango cha uzoaji taka Nlngumu kwa manispaa kwa kununua vifaa vya ubebaji taka kama magari na mitambo,Kiasi cha sh.billioni 3.02 kimetengwa,Ujenzi wa Mabweni ya Wavulana na Wasichana shule ya Sekondari Goba sh.Millioni 230 zimetengwa,"amesema.

 Akiizungumzia zaidi bajeti hiyo amesema halmashauri itatoa mikopo kwa Vikundi vya Wanawake,Vijana na Walemavu ambapo Sh.billioni 1.38 zimetengwa. Pia kupima maeneo ya Umma,kwa kutoa hati miliki na kutwaa Maeneo ya miradi ya uwekezaji Sh.billioni 1.4 zimetengwa

Amesema bajeti hiyo itajikita pia kuboresha na kujenga niundombinu ya elimu msingi na Sekondari kwa kujenga madarasa na Nyumba za walimu, ambapo sh. billioni 1.168 zimetengwa kwa kazi hiyo.

Meya amesisitiza kuwa,Halmashauri ni chombo cha wananchi ambacho kimewekwa kisheria katika kukuza uchumi na kusogeza ajira kwa Vijana ili kupunguza Umasikini hasa wa kipato ili Kujiletea Maisha Bora.
 Mkuu wa wilaya ya Ubungo,Kisare Mkori akizungumza na  Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya hiyo  waliofika  katika mkutano wa  baraza la Madiwani la kupitisha  Bajeti ya 2019/2020 leo jijini Dar es Salaam.
 Mstahiki Meya wa Halmashauri  Manispaa ya Ubungo,Boniface Jacob (kulia) akisoma hotuba yake  katika mkutano wa kupitisha bajeti ya mwa 2019-2020 leo jijini Dar es Salaam.(kushoto) Mkuu wa wilaya ya Ubungo,Kisare Mkori
 Mkurugenzi wa wa Halmashauri ya Manispaa ya  Ubungo,Betrice (kulia) akizungumza  Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya hiyo  katika mkutano wa kupitisha bajeti ya Julai,2019-Juni,2020 leo jijini Dar es Salaam.
 .Mkuu wa wilaya ya Ubungo,Kisare Makori (Kushoto) akiteta jambo Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo,Boniface Jacob wakati wa mkutano  wa  baraza la Madiwani la kupitisha  Bajeti ya 2019/2020 leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka,MMG)
Madiwani wa Halmashauri wilaya ya Bungo  waliofika katika mkutano wa  kupitisha  Bajeti ya 2019/2020 wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Ubungo,Kisare Makori.


Hivyo makala UBUNGO WACHAMBUA BAJETI YAO YA FEDHA,WAJIPANGA KUBORESHA UTOAJI HUDUMA KWA JAMII

yaani makala yote UBUNGO WACHAMBUA BAJETI YAO YA FEDHA,WAJIPANGA KUBORESHA UTOAJI HUDUMA KWA JAMII Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala UBUNGO WACHAMBUA BAJETI YAO YA FEDHA,WAJIPANGA KUBORESHA UTOAJI HUDUMA KWA JAMII mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2019/02/ubungo-wachambua-bajeti-yao-ya.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "UBUNGO WACHAMBUA BAJETI YAO YA FEDHA,WAJIPANGA KUBORESHA UTOAJI HUDUMA KWA JAMII"

Post a Comment