Polisi kanda maalumu ya DSM Yakamata Silaha Aina ya ShortGun na Watuhumiwa 14 wa Wizi wa Magari

Polisi kanda maalumu ya DSM Yakamata Silaha Aina ya ShortGun na Watuhumiwa 14 wa Wizi wa Magari - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Polisi kanda maalumu ya DSM Yakamata Silaha Aina ya ShortGun na Watuhumiwa 14 wa Wizi wa Magari, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Polisi kanda maalumu ya DSM Yakamata Silaha Aina ya ShortGun na Watuhumiwa 14 wa Wizi wa Magari
kiungo : Polisi kanda maalumu ya DSM Yakamata Silaha Aina ya ShortGun na Watuhumiwa 14 wa Wizi wa Magari

soma pia


Polisi kanda maalumu ya DSM Yakamata Silaha Aina ya ShortGun na Watuhumiwa 14 wa Wizi wa Magari

 
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam limefanikiwa kukamata silaha moja aina ya Short Gun, risasi nne za short gun na mlipuko moja uliotengenezwa kienyeji.


Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, LIBERATUS SABAS-DCP ametoa taarifa hiyo mbele ya waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, amesema Silaha hiyo ilikamatwa tarehe 25 Oktoba 2018 majira ya saa 21:30 huko maeneo ya Kijichi. Askari wakiwa doria waliitilia mashaka pikipiki iliyokuwa haina namba za usajili ikiendeshwa na kijana mmoja akiwa amewapakia wenzake wawili.

Vijana hao baada ya kutambua kuwa wanafuatiliwa na Polisi walianza kuwafyatulia risasi huku wakikimbia, ndipo askari walipojibu mapigo na kufanikiwa kumjeruhi kijana mmoja na kupelekea kufariki akiwa anapelekwa hospitali.

Kijana huyo alipekuliwa na kukutwa akiwa na silaha aina ya Shotgun iliyokatwa mtutu na kitako ikiwa na risasi nne pamoja na mlipuko mmoja.

Msako mkali unaendelea kuwasaka watuhumiwa wote waliotoroka ikiwa ni pamoja na wahalifu wengine wanaofanya matukio ya kihalifu kwa kutumia silaha za moto ndani ya jiji la Dar es Salaam.

Katika tukio lingine, Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam huko maeneo ya Kijichi limefanikiwa kukamata silaha ndogo bastola aina ya Star ambayo haikuwa na namba za usajili na risasi nne ndani ya magazine.

Katika tukio hilo lililotokea tarehe 1 Novemba 2018 majira ya saa 22:15 huko maeneo ya Kijichi Mgeninani askari wakiwa doria walitilia mashaka waendesha pikipiki yenye usajili wa namba MC 854 BBY aina ya TVS iliyokuwa ikiendeshwa na mtu mmoja huku akiwa amepakia watu wengine wawili.

Askari walipowasimamisha watu hao walikataa kutii amri halali na ghafla watu hao walifyatua risasi hewani ndipo Polisi walijibu mapigo na kuwajeruhi majambazi hao ambao walifariki wakiwa wanapatiwa matibabu hospitalini. Watu hao walipekuliwa na kukutwa na silaha hiyo.

Kukamatwa kwa mtandandao wa wizi wa magari
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watuhumiwa 14 kwa tuhuma za wizi wa magari.

Watuhumiwa hao wamekamatwa sehemu mbalimbali hapa jijini Dar es Salaam na mikoa mingine wakiwa na magari 7, Bajaji moja na pikipiki moja ya wizi vyote vimeibwa maeno mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam.

Watuhumiwa hao ni Luckman Ramadhani (36 , Ignasi Faustine (35), Ally Shaweji (30), Stephen Mwanzalima (43), Emmanuel Mabula (42), Dismas Mfoyi (32), Nyamuhanga Matiko (29), Freeman Paul (35), Ayubu Makame (41), Erasto Nyamboneke (35), Seleman Saidi (42), Dickson Mbembaji (32), Ally Rashidi (35) na Robert Nassoro (46)

Magari yaliyokamatwa ni T 162 BLW Toyota land Cruiser MALI YA UWT-TANZANIA, STL 6434 Toyota Land Cruise MALI YA WIZARA YA AFYA, T 855 DLE Toyota Harrier, T 199 DEU Toyota Noah, T 249 DLL Toyota IST, T 255 AJG Rav4 gari hii ILIIBIWA udsm IKIWA na namba T 271 DFF, T 556 DJQ Toyota Allion ,  MC 854 BYY pikipiki aina ya  TVS Honda , MC 639 BYA Bajaji

Aidha kuna magari zaidi ya manne ambayo yamekamatwa mikoani, na yako njiani yanaletwa hapa jijini Dar es salaam kwa ajili ya uchunguzi na utambuzi.

Watuhumiwa wanahojiwa na watafikishwa mahamani kwa hatua zaidi. Jeshi la polisi linaendelea na msako mkali dhidi ya wezi wa magari na watuhumiwa wengine.


Hivyo makala Polisi kanda maalumu ya DSM Yakamata Silaha Aina ya ShortGun na Watuhumiwa 14 wa Wizi wa Magari

yaani makala yote Polisi kanda maalumu ya DSM Yakamata Silaha Aina ya ShortGun na Watuhumiwa 14 wa Wizi wa Magari Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Polisi kanda maalumu ya DSM Yakamata Silaha Aina ya ShortGun na Watuhumiwa 14 wa Wizi wa Magari mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/11/polisi-kanda-maalumu-ya-dsm-yakamata.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Polisi kanda maalumu ya DSM Yakamata Silaha Aina ya ShortGun na Watuhumiwa 14 wa Wizi wa Magari"

Post a Comment