title : TRA YAWATAKA WENYE VIWANDA KUTOA TAKWIMU SAHIHI ZA UZALISHAJI WAO
kiungo : TRA YAWATAKA WENYE VIWANDA KUTOA TAKWIMU SAHIHI ZA UZALISHAJI WAO
TRA YAWATAKA WENYE VIWANDA KUTOA TAKWIMU SAHIHI ZA UZALISHAJI WAO
Mwambawahabari
wa Kodi za Ndani Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Elijah
Mwandumbya (katikati) akitoa maagizo kwa uongozi wa Kiwanda cha Manyara
Sugar Company Limited kuhusu kutoa takwimu sahihi uzalishaji sukari
wakati alipofanya ziara ya kikazi kusikiliza changamoto za
Wafanyabiashara.
Na. Rachel Mkundai, Manyara
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewataka wafanyabiashara wenye viwanda vya kutengeneza mali ghafi za kutengenezea pombe kali kutoa tawimu sahihi ya kiasi kinachozalishwa na mahali inapouzwa ili serikali iweze kukusanya kodi yake stahiki kupitia pombe kali.
Hayo yamesemwa na Kamishna waKodi za Ndani wa TRA Bw Elijah Mwandumbya mara baada ya kutembelea kiwanda cha kutengeneza sukari cha Manyara Sugar Company Limited kilichopo mkoani Manyara na kuongeza kuwa takwimu hizo zitawezesha TRA kufuatilia kwa karibu na kupata takwimu sahihi za kikodi na kuongeza makusanyo ya mapato.
“Tunafahamu kwamba “Molasis” au mali ghafi inayotokana na zao la miwa baada ya kutengeneza sukari ni bidhaa inayotumika kutengenezea pombe kali na hivyo takwimu zitatuwezesha kufuatilia wafanyabiashara wanaonunua bidhaa hiyo na kutengenezea pombe kali ili nasi tukadai kodi yetu na kodi hiyo ilete tija kwa taifa”, amesema Bw. Mwandumbya
Naye Mkuu wa mkoa wa Manyara Bw. Alexander Mnyeti amesema mkoa una mkakati wa kuongeza viwanda vingi vikubwa na vidogo ili viweze kuleta tija kwa mkoa kwa kuongeza ajira na pato la taifa kwa ujumla.
“Tunataka kuongeza viwanda vingi katika mkoa wetu ili serikali iweze kupata kodi zaidi na kuongeza mapato kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wetu”, amesema Bw. Mnyeti.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa kiwanda cha sukari cha Manyara Sugar Company Limited, Bw. Pratap Sisudya ameshukuru ujio wa Kamishna wa kodi za ndani na kuahidi kushirikiana na TRA kuhakikisha kuwa wanalipa kodi zote kwa wakati pamoja na kutoa takwimu sahihi za uzalishaji wa kiwanda.
“Ni wajibu wetu kutoa taarifa zahihi kwa TRA pamoja na kulipakodi stahiki kwa wakati ambapo kwa mwaka 2017/2018 tumelipa kodi kwa serikali takribani Shilingi bilioni 1”, alisema Bw. Sisudya.
Kiwanda cha Manyara Sugar Company kinazalisha zaidi ya tani 4,000 za sukari kwa mwaka na kina mashamba ya miwa ekari 1,600 na kutoa ajira za muda kwa watu 350 hadi 400 kwa siku.
Hivyo makala TRA YAWATAKA WENYE VIWANDA KUTOA TAKWIMU SAHIHI ZA UZALISHAJI WAO
yaani makala yote TRA YAWATAKA WENYE VIWANDA KUTOA TAKWIMU SAHIHI ZA UZALISHAJI WAO Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala TRA YAWATAKA WENYE VIWANDA KUTOA TAKWIMU SAHIHI ZA UZALISHAJI WAO mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/07/tra-yawataka-wenye-viwanda-kutoa_20.html
0 Response to "TRA YAWATAKA WENYE VIWANDA KUTOA TAKWIMU SAHIHI ZA UZALISHAJI WAO"
Post a Comment