KAMATI YA NIDHAMU TFF YAMFUNGIA JUMA NYOSO, KUKOSA MECHI TANO

KAMATI YA NIDHAMU TFF YAMFUNGIA JUMA NYOSO, KUKOSA MECHI TANO - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa KAMATI YA NIDHAMU TFF YAMFUNGIA JUMA NYOSO, KUKOSA MECHI TANO, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : KAMATI YA NIDHAMU TFF YAMFUNGIA JUMA NYOSO, KUKOSA MECHI TANO
kiungo : KAMATI YA NIDHAMU TFF YAMFUNGIA JUMA NYOSO, KUKOSA MECHI TANO

soma pia


KAMATI YA NIDHAMU TFF YAMFUNGIA JUMA NYOSO, KUKOSA MECHI TANO

Na Zainab Nyamka,Globu ya Jamii.

KAMATI ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imetangaza kumfungia  Juma Nyoso wa Kagera Sugar kwa kosa la kupiga shabiki baada ya mchezo kati ya timu yake dhidi ya Simba kwenye uwanja wa Kaitaba, mkoani Kagera.

Akitolea ufafanuzi hukumu hiyo, Ofisa habari wa TFF Clifford Ndimbo amesema kamati ya nidhamu iliketi na kujadili masuala mbalimbali ya nidhamu ikiwemo suala la beki wa timu ya Kagera Juma Nyoso kumpiga shabiki wakati wa mchezo wao dhidi ya Simba uliochezwa mwanzoni mwa mwaka huu.

Ndimbo amesema  "Kamati ya nidhamu ya TFF iliweza kukaa na kulijadili masuala mbalimbali ya nidhamu pia  ilijadili shauri ambalo lilifikishwa kwenye kamati hiyo ambalo lilimuhusu mchezaji wa Kagera Sugar Juma Nyoso kuhusu tukio lake ambalo lilitokea kwenye mchezo uliozikutanisha Kagera Sugar na Simba kwenye uwanja wa Kaitaba," amesema.

Katika kesi hiyo Nyoso alituhumiwa kwa kosa la kumpiga shabiki na kupelekea kupoteza fahamu baada ya kumalizika kwa mchezo kinyume na kanuni za ligi kuu zinazozungumzia uungwana katika mchezo wa kosa 'Fair Play'.

Katika hukumu hiyo iliyotolewa na Kamati waliweza kupitia ripoti ya kamishna wa mchezo huo ambapo imeweza kuelezea  tukio hilo ambapo  Nyoso wakati anaelekea vyumbani aliweza kupishana na shabiki aliyekuwa anapuliza vuvuzela na kusababisha Nyoso kusimama na kuanza kumpiga shabiki huyo kwa kutumia kiatu na baadaye akamuinamisha na kuanza kumpiga kwa kutumia goti.

"Kwa upande wa Kamati iliweza kumuita Nyoso na kujitetea na kwa upande wake alikana madai yanayomkabili ya kumpiga shabiki na kudai kuwa amlikunja na sio kumpiga," amesema Ndimbo

Baada ya kumsikiliza utetezi wake Kamati imeweza kumtia hatiani Nyoso kwa kupitia kanuni ya ligi kuu na pia waliweza kupitia  taarifa za nyuma za mchezaji huyo na kuona kuwa Nyoso  aliwahi kuadhibiwa kwa makosa ya utovu wa nidhamu. 

Nyoso amepewa adhabu ya kukosa mechi tano na faini ya Sh.milioni moja.


Hivyo makala KAMATI YA NIDHAMU TFF YAMFUNGIA JUMA NYOSO, KUKOSA MECHI TANO

yaani makala yote KAMATI YA NIDHAMU TFF YAMFUNGIA JUMA NYOSO, KUKOSA MECHI TANO Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala KAMATI YA NIDHAMU TFF YAMFUNGIA JUMA NYOSO, KUKOSA MECHI TANO mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/02/kamati-ya-nidhamu-tff-yamfungia-juma.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "KAMATI YA NIDHAMU TFF YAMFUNGIA JUMA NYOSO, KUKOSA MECHI TANO"

Post a Comment