title : SERIKALI KUBORESHA VITUO VYA AFYA.
kiungo : SERIKALI KUBORESHA VITUO VYA AFYA.
SERIKALI KUBORESHA VITUO VYA AFYA.
MwambawahabariAngela Msimbira OR TAMISEMI LINDI
Serikali inaendelea kutekeleza Mkakati wa kuviboresha na kujenga vituo vya afya nchini ili viweze kutoa huduma bora inayoendana na mahitaji halisi ya wananchi suala ambalo ni mpango wanne wa Sekta ya afya (HSSP-IV).
Hayo yamebainishwa leo na Msimamizi wa Kitengo cha Dawa Vifaa, Vifaa tiba , vitendanishi na huduma za kichuhuzi za Afya kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Bw. Mathew Mganga wakati akiongea na Wafanyakazi wa Kituo cha afya cha Nkoe kilichopo kilichopo katika Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi.
Bw. Mathew Mganga amesema kuwa Katika kutekeleza lengo hilo Serikali na Wadau wa Maendeleo wanashirikiana katika ukarabati miundombinu iliyopo na kujenga miundombinu mipya ya vituo vya kutolea huduma za Afya kwenye vituo vya afya, Zahanati na Hospitali kwa lengo la kutoa huduma bora kwa wananchi.
Amesema serikali imekuja na makakati wa kupeleka fedha kwenye vituo vya afya ambavyo vilikuwa havitoi huduma mbalimbali za afya ziweze kutoa huduma hizo kwa wananchi.
Fedha hizo zimelenga kukarabati au kujenga katika maeneo ya vipaumbele kama ifuatavyo: Jengo la upasuaji, wodi ya akina mama, wodi ya wototo, Maabara, Nyumba za watumishi inayojitegemea, Chumba cha kuifadhia maiti, Kichomea taka na shimo la kuchomea Kondo la Nyuma, Mfumo wa ukusanyaji wa maji ya mvua na vifaa na vifaa tiba kwenye vituo vya kutolea huduma.
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi katika kituo cha afya Nkoe,Wilayani Ruangwa Bw. Mohamedi Pilipili ameishukuru Serikali kwa kutoa shilingi milioni 500 kwa ajili ya kujenga miundombinu ya afya katika wilaya hiyo.
Amesema awali kituo cha afya cha Nkoe kilikuwa katika hali mbaya ya uchakavu wa majengo, kutokuwa na chumba cha upasuaji, maabara, wodi ya wazazi na watoto pamoja na chumba cha kuifazia maiti jambo ambalo kwa hivi sasa limeweza kutatuliwa kwa kujengwa ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma za afya katika kituo hicho.
Amesema kuwa wananchi wameweza kuchimba msingi pamoja na kuchota mchanga ili kuhakikisha Kituo cha afya kinajengwa kwa wakati na kupunguza changamoto zilizokuwepo za miundombinu ya afya katika Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi.
Aidha Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OT-TAMISEMI) kwa kushirikiana ofisi ya Waziri Mkuu, na Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora zinafanya ufuatiliaji wa maendeleo ya ujenzi na ukarabatiwapo wa vituo vya afya kwenye Mikoa na Halmashauri zote zinazotekeleza miradi ya afya nchini.
Hivyo makala SERIKALI KUBORESHA VITUO VYA AFYA.
yaani makala yote SERIKALI KUBORESHA VITUO VYA AFYA. Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala SERIKALI KUBORESHA VITUO VYA AFYA. mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/01/serikali-kuboresha-vituo-vya-afya.html
0 Response to "SERIKALI KUBORESHA VITUO VYA AFYA."
Post a Comment