Kituo Cha Afya Chalinze Chaanza Kufawanyia Oparesheni Wagonjwa

Kituo Cha Afya Chalinze Chaanza Kufawanyia Oparesheni Wagonjwa - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Kituo Cha Afya Chalinze Chaanza Kufawanyia Oparesheni Wagonjwa, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Kituo Cha Afya Chalinze Chaanza Kufawanyia Oparesheni Wagonjwa
kiungo : Kituo Cha Afya Chalinze Chaanza Kufawanyia Oparesheni Wagonjwa

soma pia


Kituo Cha Afya Chalinze Chaanza Kufawanyia Oparesheni Wagonjwa

Na Omary Mngindo, Lugoba

KITUO cha afya cha Chalinze kilichopo Kitongoji cha Bwilingu halmashauri ya Chalinze Bagamoyo Mkoa wa Pwani kimeanza kuwafanyia operesheni wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo kituoni hapo.

Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Mwanasheria Ridhiwani Kikwete ndiye aliyechokonoa hoja hiyo alipomtaka Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo kumpatia uhakika wa jambo hilo ambalo analisikia kwa watu kwamba Kituo hicho kimeshaanza zoezi la kuwafanyia upasuaji wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo.

"Nimesikia maneno kutoka kwa wakazi wakisema kwamba Kituo chetu cha afya Chalinze kimeshaanza kuwafanyia upasuaji wagonjwa wanaokwenda kwa ajili ya huduma hiyo, Mganga Mkuu tunaomba ulitaarifu Baraza hili taarifa hizo zilizo njema zina ukweli gani?," aliuliza Ridhiwani.

Akijibu swali hilo, Dr. Isaack Makungu aliwathibitishia Madiwani hao kwamba taarifa hizo zina ukweli na tayari akina mama 10 wajawazito wameshapatiwa huduma ya upasuaji kisha kupata watoto wakiwa salama na afya njema pamoja na wazazi wenyewe wakiwa na afya iliyo njema.

"Ni kweli Kituo chetu kimeshaanza kazi ya kuwafanyia upasuaji akina mama wajawazito ambao wamebainika hawana uwezo wa kusukuma mtoto ambapo watu kumi tumeshawapatia huduma hiyo wakiwa salama wao pamlja na watoto wao," alisema Dr. Makungu.

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Said Zikatimu aliliambia Baraza hilo kwamba hatua hiyo ni faraja kwao kwani itasaidia mambo mengi kwanza kuwapunguzia saafari ndefu ya kwenda Tumbi, Bagamoyo au Muhimbili, poa mafuta ambayo yalikuwa yanatumika kusafirisha wagonjwa kweda maeneo nayo.

"Taarifa hiyo ni faraja kwetu kwani itasaidia wagonjwa ambao awali walikuwa wanasafirishwa kwenda Tumbi, Bagamoyo au Muhimbili, lakini tunatakiwa kujenga uzio kutoka chumba cha upasuaji kwenda wodini ili mgonjwa anapotoka kufanyiwa upauaji asiwe anaonekana na watu wengine," alisema Zikatimu.


Hivyo makala Kituo Cha Afya Chalinze Chaanza Kufawanyia Oparesheni Wagonjwa

yaani makala yote Kituo Cha Afya Chalinze Chaanza Kufawanyia Oparesheni Wagonjwa Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Kituo Cha Afya Chalinze Chaanza Kufawanyia Oparesheni Wagonjwa mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/08/kituo-cha-afya-chalinze-chaanza.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Kituo Cha Afya Chalinze Chaanza Kufawanyia Oparesheni Wagonjwa"

Post a Comment