title : Muhimbili tawi la Mloganzila yaadhimisha siku ya Ukimwi Duniani kwa kutoa huduma ya upimaji wa afya bure
kiungo : Muhimbili tawi la Mloganzila yaadhimisha siku ya Ukimwi Duniani kwa kutoa huduma ya upimaji wa afya bure
Muhimbili tawi la Mloganzila yaadhimisha siku ya Ukimwi Duniani kwa kutoa huduma ya upimaji wa afya bure
Muhimbili tawi la Mloganzila yaadhimisha siku ya Ukimwi Duniani kwa kutoa huduma ya upimaji wa afya bure. Mamia ya wananchi leo wamejitokeza kupima afya zao katika Hospitali ya Taifa Muhimbili tawi la Mloganzila iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani ambapo hospitali hiyo imefanya zoezi la upimaji bure pamoja na kutoa ushauri nasaha.
Akizungumza katika maadhimisho hayo ambayo yamefadhiliwa na kampuni ya HETERO Laboratories, Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Tawi la Mloganzila Dkt. Julieth Magandi amesema takwimu zinaonesha kuwa kila watanzania mia moja watu 4.7 wenye umri kati ya miaka 15 hadi 49 kati yao wameathirika na Virusi vya Ukimwi na takribani watanzania 1.4 milioni wanaishi na Virusi vya Ukimwi.
Pia kwa mujibu wa Shirika la afya duniani -WHO-, watu milioni 37 duniani wanaishi na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi huku vijana wakiendelea kuwa kundi lililoko hatarini zaidi kuambukizwa VVU hasa barani Afrika.
Akielezea kuhusu mafanikio ya utoaji huduma katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Dkt. Magandi amesema Muhimbili hutoa huduma za VVU katika kliniki zake za wagonjwa wa nje kila siku ambapo wagonjwa 3,534 wanahudumiwa, huku Hospitali ya Taifa Muhimbili tawi la Mloganzila ikihudumia takribani wagonjwa 70.
Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Tawi la Mloganzila Dkt. Julieth Magandi akifungua maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani ambapo Muhimbili-tawi la Mloganzila imeadhimisha siku hiyo leo kwa kutoa huduma ya upimaji bure.
Baadhi ya wananchi ambao wamejitokeza kwa ajili ya kupata huduma wakimsikiliza Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji wakati wa ufunguzi wa maadhimisho hayo.
Daktari Bingwa wa magonjwa ya ndani ambaye pia ni Mkuu wa kitengo cha magonjwa ya kuambukiza katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Dkt. Amina Mgunja akitoa elimu kwa wananchi kuhusu ugonjwa wa Ukimwi.
Hivyo makala Muhimbili tawi la Mloganzila yaadhimisha siku ya Ukimwi Duniani kwa kutoa huduma ya upimaji wa afya bure
yaani makala yote Muhimbili tawi la Mloganzila yaadhimisha siku ya Ukimwi Duniani kwa kutoa huduma ya upimaji wa afya bure Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Muhimbili tawi la Mloganzila yaadhimisha siku ya Ukimwi Duniani kwa kutoa huduma ya upimaji wa afya bure mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/12/muhimbili-tawi-la-mloganzila.html
0 Response to "Muhimbili tawi la Mloganzila yaadhimisha siku ya Ukimwi Duniani kwa kutoa huduma ya upimaji wa afya bure"
Post a Comment