title : HOSPITAL ya Amana kutibia bure wagonjwa wa meno
kiungo : HOSPITAL ya Amana kutibia bure wagonjwa wa meno
HOSPITAL ya Amana kutibia bure wagonjwa wa meno
Mganga mkuu wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa Amana Dkt Meshack Shimwela (Katikati) akiwa na Muuguzi Mkuu wa Amana Beauty Mwabebule na wauguzi wengine Dar es Salam leo wakati wa ufunguzi wa utoaji wa huduma bure ya kinywa na meno kwa muda wa siku tatu Picha na Heri Shaban
Na Heri Shaban
Mwambawahabari
HOSPITAL ya Rufaa ya Mkoa Amana imetenga siku tatu ya wiki ya kuhudumia wagonjwa wa meno na kinywa bure.
Hayo yalisemwa Dar es Salam leo na Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa Amana Mkoa Dar es Salam Dkt. Meshack Shimwela katika wiki maalum ya hospitali hiyo.
"Katika hospitali yetu ya Amana ambayo kwa sasa ni ya Rufaa tumetenga siku tatu za kuhudumia wagonjwa wa meno bure kuwapatia Matibabu katika hospitali yetu amewataka Wananchi kujitokeza kupatiwa tiba "alisema Dkt. Shimwela.
Dkt.Shimwela alisema yeye na timu yake wiki hii ya Amana HOSPITAL wamependekeza kutibia wagonjwa wa meno bure ambapo mgonjwa akitibiwa na kupatiwa tiba kama anaugonjwa mwingine unaoneka kupitia vipimo vyao.
Alisema siku ya kufunga kesho kutwa huduma hiyo ya tiba ya meno itamia katika hospitali ya Mnazi Mmoja dhumuni lake kuwafikia Wananchi 5000.
Akielezea utoaji huduma katika hospitali hiyo alisema kwa siku wagonjwa 700 na Upasuaji wagonjwa 15 hadi 70 kwa siku.
Pia alielezea mafanikio ya hospitali hiyo katika miaka mitatu ya Rais Magufuli Amana kwa sasa ni Hospitali ya Rufaa na huduma za kisasa pamoja na Wauguzi Mabingwa katika Mkoa wa Dar es Salam ni hospitali ya kwanza ya Serikali inatoa huduma Mfumo wa Kisasa.
Mafanikio mengine dawa zinapatikana za kutosha asilimia 90 dawa zipo wagonjwa wote wanapewa dawa ndani ya jengo hilo.
Kwa upande wake Muuguzi Mkuu wa HOSPITAL ya Rufaa Amana Beauty Mwambebule alisema katika hosptali hiyo kwa siku wanajifungua Wanawake 70 hadi 80 na vifo vya Mama na Mtoto kwa sasa ni asilimia 20 vimepungua.
Mwambebule aliwataka wamama Wajawazito kuwai Kliniki mapema na katika vituo vya afya ili kujua tarehe ya kujifungua lengo kupunguza vifo vya Mama na Mtoto.
Pia alisema hospitali hiyo ni ya Rufaa wanapokea wagonjwa kwa taarifa kabla ujafika Amana Wauguzi na Daktari wanakuwa wameshaweka maandalizi ya kumpokea mgonjwa na dawa zake katika chumba maalum kwa wagonjwa wa zarula.
Akizungumzia Malalamiko kwa watumishi amesema wanapatiwa mafunzo endelevu na Serikali ya Maadili kwa ajili ya kuwajenga.
Hivyo makala HOSPITAL ya Amana kutibia bure wagonjwa wa meno
yaani makala yote HOSPITAL ya Amana kutibia bure wagonjwa wa meno Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala HOSPITAL ya Amana kutibia bure wagonjwa wa meno mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/12/hospital-ya-amana-kutibia-bure-wagonjwa.html
0 Response to "HOSPITAL ya Amana kutibia bure wagonjwa wa meno"
Post a Comment