DC MJEMA ATOA SOMO KWA WAZAZI ,WALEZI KUPOROMOKA KWA MAADILI,AZITAKA SHULE BINAFSI KUSHIRIKIANA NA ZA SERIKALI.

DC MJEMA ATOA SOMO KWA WAZAZI ,WALEZI KUPOROMOKA KWA MAADILI,AZITAKA SHULE BINAFSI KUSHIRIKIANA NA ZA SERIKALI. - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa DC MJEMA ATOA SOMO KWA WAZAZI ,WALEZI KUPOROMOKA KWA MAADILI,AZITAKA SHULE BINAFSI KUSHIRIKIANA NA ZA SERIKALI., tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : DC MJEMA ATOA SOMO KWA WAZAZI ,WALEZI KUPOROMOKA KWA MAADILI,AZITAKA SHULE BINAFSI KUSHIRIKIANA NA ZA SERIKALI.
kiungo : DC MJEMA ATOA SOMO KWA WAZAZI ,WALEZI KUPOROMOKA KWA MAADILI,AZITAKA SHULE BINAFSI KUSHIRIKIANA NA ZA SERIKALI.

soma pia


DC MJEMA ATOA SOMO KWA WAZAZI ,WALEZI KUPOROMOKA KWA MAADILI,AZITAKA SHULE BINAFSI KUSHIRIKIANA NA ZA SERIKALI.



Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe.Sophia  (Nakivona ) Mjema  akiwatunuku vyeti wahitimu wa Darasa la saba katika mahafali ya 24 ya shule ya  msingi TUSIIME ambapo jumla yawanafunzi  245  wamehimu elimu ya Msingi.( Picha na Mwamba wa habari)


 Mmoja wa wazazi waliofika katika sherhe za mahali ya darasa la saba shuke ya msingi TUSIIME akimtunza DC Mjema baada ya kuguswa na hotuba yake kuhusu malezi ya watoto na kushindwa kujizuia na  kujikuta akitoa pochi na kutuza , DC mjema alitoa hotuba ambayo iligusa wazazi  na wanafunzi.


Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe.Sophia  Mjema akimpa zawadimoja wa  wanafuzi waliofanya vizuri katika mitihani.


Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe.Sophia  Mjema akishukuru baada ya kupewa zawadi zawadi katika shule ya TUSIIME.

Na.John Luhende 
Mwamba wa habari.
Wazazi na walezi wametakiwa kuwa karibu na kufuatilia malezi ya watoto wao ilikuwajengea watoto msingi mzuri kimaisha moyo wa upendo jambo ambalo litawasaidia hata katika masomoyao waweze kufanya vizuri , kuwa wazalendo na raia wema katika Taifa.

Wito huo umetolewa na mkuu wa Wilaya ya Ilala alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali  ya darasa la saba katika shule ya tusiime , na kuongeza kuwa watoto wengi wamengi wamekuwa na tabia mbaya  kwa kukosa malezi ya familia  na kuiga mambo ya kimagharibi  na kuaziacha tamaduni za kitanzania jambo ambalo limechangia kuporomoka kwa maadili.

‘’Upendo wa familia unajengwa kwa familia kujumuika pamoja katika chakula cha jioni , Baba , Mama na Watoto  na sikuiga mabo ya nje huko unakuta Wazi wako bize na mitandao ya kijamii na unakuta mwingine anawekewa chakula chumbani hayo siyo malezi, upendo nipale mnapokula  katika mzunguko wa pamoja huyu anasema niongezee  kawali ,Mamaniwekee juisi  ,nibora wazazi tukatenga huo muda "alisema.

Aidha DC mjema amekemea vikali tabia za kuiga kutoka nchi zanje kila jambo kwa kuwa kuna mambo mengine yanayoigwa hana staha na heshima kwa  jamii za kitanzania kwani mambo hayo yanachangia uharifu na uvunjifu wa maadili.

‘’ Kuna hiki kitu kina itwa sleep over sijui summer paty,vitu gani hivi  vya kuiga vinatuharibia maadili ya watoto unakuta wanaalikana njoo na nightdress mzazi unajua wanaenda kufanya nini huko?  Dont do that ,nasema hakuna sleep over hakuna kwa ninyi waswahili ni marufuku’’alionya DC Mjema .

DC Mjema pia amewataka wazazi kuwa waangalifu na watoto wao waliomaliza darasa la saba kwa kipindi hiki wakati wanangoja mhula wa kujiunga na kidato cha kwanza  ili wasije kujiingiza katika makundi mabaya na kuangukia katika mikondo ya watu waharifu wakazimandotozao za kuendelea na masomo.

” Wazazi watoto hawa msiwaacha wakaanza kuzurula kuna simba huko watawararula usikubali kumwancha mtoto zaidi ya dakika tano bila kufahamu yuko wapi na anafanya nini , na ninyi watoto  mtulie muache kuzurula hovyo “ alisema .

Pamoja na hayo  DC Mjema amesema serikali  ya awamu ya tano katika kuboresha elimu na kutoa fursa kwa kilamtoto wa Tanzania kupata elimu , imeamnua kutoa elimu bure  na inaendelea kuboresha maslahai ya walimu ili kuinua kiwango cha elimu na amewataka wamiliki wa shule binafsi  wilayani Ilala kushirikiana na shule za serikali kitaaluma na katika michezo  kwani  pamoja na kwamba shule zao ni za kulipia  lakini wate wanajenga Taifa moja.

‘’Ninyi Tusiime mnao uwezo shirikianeni shule zetu za serikali  mnzo maabara nzuri  wakaribisheni wanafunzi na walimu wetu kujifunza hapa kwenu, pia natoa wito kwa shule zote zilizopo wilaya ya Ilala kuzingatia ratiba za michezo kwa watoto ilikuimarisha afya na kuvumbua vipaji vyao naninyi tusiime mpo mkiona shule zetu zinazubaa shulezetu zinajikongoja  ingieni na waambieni mtafanya mashindano na kutoa mipira  na viwanja  nnaweza.''alisema

Kwa upande wake Mwalimu kuu wa shule ya Tusiime Philibert Simon , amesema shule hiyo imetatoa bure saili wa kidato cha kwanza kwa wahimu wa darasa la saba walio hitimu katika shule hiyo.

Shule ya TUSIIME ilianzishwa  zaidi ya miaka  20 iliyopita  na imepata mafanikio makubwa  katika Nyanja mbalimbali hasa kitaaluma, ambapo  kwa kipindi chote hicho  imeendelea kufanya vizuri katika mitihani ya ndani,  mitahani ya kata ,  mitihani ya Wilaya , Mkoa na Taifa  ambapo mwaka jana katika matokeo ya kumaliza Elimu ya Msingi ilishika nafasi ya 20 katiya shule 16,545 na kushika nafasi yatatu kimkoa na nafasi ya kwanza kiwilaya (Ilala) na mwanafunzi bora  pia alitoka TUSIIME na kwa upande wa wasichana kumi bora mmoja alitoka shulehiyo.



Hivyo makala DC MJEMA ATOA SOMO KWA WAZAZI ,WALEZI KUPOROMOKA KWA MAADILI,AZITAKA SHULE BINAFSI KUSHIRIKIANA NA ZA SERIKALI.

yaani makala yote DC MJEMA ATOA SOMO KWA WAZAZI ,WALEZI KUPOROMOKA KWA MAADILI,AZITAKA SHULE BINAFSI KUSHIRIKIANA NA ZA SERIKALI. Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala DC MJEMA ATOA SOMO KWA WAZAZI ,WALEZI KUPOROMOKA KWA MAADILI,AZITAKA SHULE BINAFSI KUSHIRIKIANA NA ZA SERIKALI. mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/10/dc-mjema-atoa-somo-kwa-wazazi-walezi.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "DC MJEMA ATOA SOMO KWA WAZAZI ,WALEZI KUPOROMOKA KWA MAADILI,AZITAKA SHULE BINAFSI KUSHIRIKIANA NA ZA SERIKALI."

Post a Comment