title : MWALIMU MKUU SHULE YA MSINGI YA KIMATAIFA HAZINA ,WALIMU WANNE KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA KUPATA MTIHANI WA TAIFA DARASA LA SABA
kiungo : MWALIMU MKUU SHULE YA MSINGI YA KIMATAIFA HAZINA ,WALIMU WANNE KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA KUPATA MTIHANI WA TAIFA DARASA LA SABA
MWALIMU MKUU SHULE YA MSINGI YA KIMATAIFA HAZINA ,WALIMU WANNE KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA KUPATA MTIHANI WA TAIFA DARASA LA SABA
Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii
MWALIMU Mkuu wa Shule ya Msingi ya Kimataifa ya Hazina iliyopo Magomeni jijini Dar es Salaam na walimu wake wanne wamepandishwa katika kizimba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Sababu za kupandishwa kizimbani inatokana na kutakiwa kujibu tuhuma za kupata mitihani ya Taifa ya darasa la saba na kufanya mawasiliano ya maudhui yake na watahiniwa wa shule hiyo isivyo halali.
Mwalimu Mkuu huyo Patrick Cheche (43) Wa shule hiyo ambayo mara kwa mara imekuwa ikitangazwa kufanya vizuri katika mitihani ya Taifa ya darasa la nne na la saba na walimu wenzake wamesomewa mashtaka yao leo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Huruma Shahidi.
Mbali na Cheche (43), anayeishi Mpinga Bagamoyo, washtakiwa wengine ni Laurence Ochien (30), Justus James (32), Nasri Mohamed (32) na Mambo Idd (32), ambao wote wakazi wa Dar es Salaam.
Akisoma hati ya mashtaka Wakili wa Serikali Mwandamizi Mutalemwa Kishenyi akisaidiana na Wakili wa Serikali, Mwanaamina Kombakono amedai washitakiwa hao Septemba 4, mwaka huu, katika Jiji na Mkoa wa Dar es Salaam kwa pamoja walikula njama ya kutenda kosa la kuingilia mitihani ya Taifa ya darasa la saba isivyo halali.
Washtakiwa katika Shtaka hilo la kula njama wanashtakiwa chini ya Sheria ya Kanuni za adhabu.
Katika shtaka la pili ambao washtakiwa hao wanashitakiwa chini ya Sheria ya Baraza la Mitihani la Taifa, wanadaiwa Septemba 5 mwaka huu katika shule hiyo ya Hazina, iliyoko Magomeni, kujibu, kinyume cha sheria walipata uwezo wa kupata mitihani wa taifa wa darasa la saba na kuonesha maudhui yake kwa watahiniwa waliosajiliwa Katina shule hiyo.
Pia imedaiwa Katika shtaka la tatu, Septemba 5 mwaka huu katika shule hiyo washtakiwa hao kwa makusudi walitoa mitihani kwa watahiniwa waliosajiliwa katika shule hiyo wakati hawakustahili kufanya hivyo.Hata hivyo washtakiwa wote wamekana kutenda kosa hilo na wako nje kwa dhamana.
Kwa Mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.Akisoma masharti ya dhamana, Hakimu Shaidi amesema ili washtakiwa wawe nje kwa dhamana, kila mmoja anatakiwa awe na wadhamini wawili wenye barua za utambulisho, vitambulisho na mmoja kati ya wadhamini hao awe anatambulika katika taasisi yoyote.
Pia kila mdhamini anatakiwa kusaini bondi ya Sh.milioni sita na mshtakiwa wa kwanza na wa pili watatakiwa kuwasilisha hati zao za kusafiria kwani wao ni raia wa Kenya.Hata hivyo washtakiwa hao walifanikiwa kukamilisha masharti hayo ya dhamana kasoro mshtakiwa wa pili ambaye alipelekwa rumande baada ya kushindwa kukamilisha masharti hayo ya dhamana.
Kesi imeahirishwa hadi Oktoba 10, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa ili kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika ama laa.
MWALIMU Mkuu wa Shule ya Msingi ya Kimataifa ya Hazina iliyopo Magomeni jijini Dar es Salaam na walimu wake wanne wamepandishwa katika kizimba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Sababu za kupandishwa kizimbani inatokana na kutakiwa kujibu tuhuma za kupata mitihani ya Taifa ya darasa la saba na kufanya mawasiliano ya maudhui yake na watahiniwa wa shule hiyo isivyo halali.
Mwalimu Mkuu huyo Patrick Cheche (43) Wa shule hiyo ambayo mara kwa mara imekuwa ikitangazwa kufanya vizuri katika mitihani ya Taifa ya darasa la nne na la saba na walimu wenzake wamesomewa mashtaka yao leo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Huruma Shahidi.
Mbali na Cheche (43), anayeishi Mpinga Bagamoyo, washtakiwa wengine ni Laurence Ochien (30), Justus James (32), Nasri Mohamed (32) na Mambo Idd (32), ambao wote wakazi wa Dar es Salaam.
Akisoma hati ya mashtaka Wakili wa Serikali Mwandamizi Mutalemwa Kishenyi akisaidiana na Wakili wa Serikali, Mwanaamina Kombakono amedai washitakiwa hao Septemba 4, mwaka huu, katika Jiji na Mkoa wa Dar es Salaam kwa pamoja walikula njama ya kutenda kosa la kuingilia mitihani ya Taifa ya darasa la saba isivyo halali.
Washtakiwa katika Shtaka hilo la kula njama wanashtakiwa chini ya Sheria ya Kanuni za adhabu.
Katika shtaka la pili ambao washtakiwa hao wanashitakiwa chini ya Sheria ya Baraza la Mitihani la Taifa, wanadaiwa Septemba 5 mwaka huu katika shule hiyo ya Hazina, iliyoko Magomeni, kujibu, kinyume cha sheria walipata uwezo wa kupata mitihani wa taifa wa darasa la saba na kuonesha maudhui yake kwa watahiniwa waliosajiliwa Katina shule hiyo.
Pia imedaiwa Katika shtaka la tatu, Septemba 5 mwaka huu katika shule hiyo washtakiwa hao kwa makusudi walitoa mitihani kwa watahiniwa waliosajiliwa katika shule hiyo wakati hawakustahili kufanya hivyo.Hata hivyo washtakiwa wote wamekana kutenda kosa hilo na wako nje kwa dhamana.
Kwa Mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.Akisoma masharti ya dhamana, Hakimu Shaidi amesema ili washtakiwa wawe nje kwa dhamana, kila mmoja anatakiwa awe na wadhamini wawili wenye barua za utambulisho, vitambulisho na mmoja kati ya wadhamini hao awe anatambulika katika taasisi yoyote.
Pia kila mdhamini anatakiwa kusaini bondi ya Sh.milioni sita na mshtakiwa wa kwanza na wa pili watatakiwa kuwasilisha hati zao za kusafiria kwani wao ni raia wa Kenya.Hata hivyo washtakiwa hao walifanikiwa kukamilisha masharti hayo ya dhamana kasoro mshtakiwa wa pili ambaye alipelekwa rumande baada ya kushindwa kukamilisha masharti hayo ya dhamana.
Kesi imeahirishwa hadi Oktoba 10, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa ili kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika ama laa.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ya Kimataifa ya Hazina iliyopo Magomeni jijini Dar es Salaam na walimu wake wanne wakipandishwa katika kizimba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mapema leo.
Hivyo makala MWALIMU MKUU SHULE YA MSINGI YA KIMATAIFA HAZINA ,WALIMU WANNE KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA KUPATA MTIHANI WA TAIFA DARASA LA SABA
yaani makala yote MWALIMU MKUU SHULE YA MSINGI YA KIMATAIFA HAZINA ,WALIMU WANNE KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA KUPATA MTIHANI WA TAIFA DARASA LA SABA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala MWALIMU MKUU SHULE YA MSINGI YA KIMATAIFA HAZINA ,WALIMU WANNE KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA KUPATA MTIHANI WA TAIFA DARASA LA SABA mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/09/mwalimu-mkuu-shule-ya-msingi-ya.html
0 Response to "MWALIMU MKUU SHULE YA MSINGI YA KIMATAIFA HAZINA ,WALIMU WANNE KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA KUPATA MTIHANI WA TAIFA DARASA LA SABA"
Post a Comment