Waziri Ndalichako akabidhi magari 47 kwa wathibiti ubora wa Shule wa Kanda na Wilaya

Waziri Ndalichako akabidhi magari 47 kwa wathibiti ubora wa Shule wa Kanda na Wilaya - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Waziri Ndalichako akabidhi magari 47 kwa wathibiti ubora wa Shule wa Kanda na Wilaya, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Waziri Ndalichako akabidhi magari 47 kwa wathibiti ubora wa Shule wa Kanda na Wilaya
kiungo : Waziri Ndalichako akabidhi magari 47 kwa wathibiti ubora wa Shule wa Kanda na Wilaya

soma pia


Waziri Ndalichako akabidhi magari 47 kwa wathibiti ubora wa Shule wa Kanda na Wilaya

 Waziri wa elimu, sayansi na teknolojia  Profesa Joyce Ndalichako akizungumza wakati wa kukabidhi magari 47 kwa ajili ya wathibiti wa  ubora wa  Shule  wa Kanda na Wilaya na magari  mawili  kwa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) katika hafla iliyofanyika hapa Mjini Dodoma.
 Waziri wa elimu, sayansi na teknolojia  Profesa Joyce Ndalichakoakikata utepe kuashiria uzinduzi wa ugawaji wa magari hayo kwawathibiti  wa ubora wa  Shule  wa Kanda na Wilaya na magari  mawili  kwa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) katika hafla iliyofanyika hapa Mjini Dodoma.
 Waziri wa elimu, sayansi na teknolojia  Profesa Joyce Ndalichako akiwa katika gari mara baada ya kuzindua
Sehemu ya magari ya wathibiti wa  ubora wa  Shule  wa Kanda na Wilaya na magari  mawili  kwa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia  Profesa Joyce Ndalichako amekabidhi magari kwa ajili ya kuimarisha Uthibiti wa ubora elimu.
Jumla ya magari hayo ni 47, ambapo  magari 45 ni kwa ajili ya wathibiti ubora wa  Shule  wa Kanda na Wilaya na magari  mawili  kwa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA).
Akizungumza wakati wa kukabidhi magari hayo mjini Dodoma Profesa Ndalichako amesema  wathibiti ubora  wa shule kutumia  magari hayo   kwa malengo yaliyokusudiwa na hatua kali zitachukuliwa kwa wale watakaotumia magari hayo kinyume na malengo yaliyokusudiwa.
Amesema kwa mujibu wa Dira yetu ya Maendeleo, Mpango wa Maendeleo wa Miaka mitano na Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020 Tanzania inalenga kujenga uchumi wa Viwanda ili kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.
Profesa Ndalichako amesema kufikia malengo ya uchumi wa kati  Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ndiyo yenye dhamana ya kusimamia utoaji elimu, ujuzi, maarifa na stadi zitakazowawezesha vijana wetu kutoa mchango unaotakiwa katika ujenzi wa uchumi wetu.
Aidha Wizara itasimamia vyema elimu na mafunzo yatolewayo ili kuhakikisha yanakuwa bora na yanatoa mchango wenye tija katika ujenzi wa uchumi wetu.  
“Ninathubutu kusema kuwa Serikali ya awamu ya tano kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inasimamia kwa dhati kabisa jukumu hili la utoaji wa elimu bora kwa kununuaa pikipiki 2,894 ambazo zimesambazwa kwenye Halmashauri 156 katika mikoa 25 kwa ajili ya kusaidia  Waratibu Elimu Kata katika kutekeleza majukumu yao ili kuhakikisha kuwa elimu bora inatolewa shuleni katika maeneo yao.


Hivyo makala Waziri Ndalichako akabidhi magari 47 kwa wathibiti ubora wa Shule wa Kanda na Wilaya

yaani makala yote Waziri Ndalichako akabidhi magari 47 kwa wathibiti ubora wa Shule wa Kanda na Wilaya Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Waziri Ndalichako akabidhi magari 47 kwa wathibiti ubora wa Shule wa Kanda na Wilaya mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/07/waziri-ndalichako-akabidhi-magari-47.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Waziri Ndalichako akabidhi magari 47 kwa wathibiti ubora wa Shule wa Kanda na Wilaya"

Post a Comment