VIJANA WA MOROGORO WANUFAIKA NA AJIRA UJENZI RELI MWENDO KASI ‘SGR’

VIJANA WA MOROGORO WANUFAIKA NA AJIRA UJENZI RELI MWENDO KASI ‘SGR’ - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa VIJANA WA MOROGORO WANUFAIKA NA AJIRA UJENZI RELI MWENDO KASI ‘SGR’, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : VIJANA WA MOROGORO WANUFAIKA NA AJIRA UJENZI RELI MWENDO KASI ‘SGR’
kiungo : VIJANA WA MOROGORO WANUFAIKA NA AJIRA UJENZI RELI MWENDO KASI ‘SGR’

soma pia


VIJANA WA MOROGORO WANUFAIKA NA AJIRA UJENZI RELI MWENDO KASI ‘SGR’

Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dk Kebwe Stephen Kebwe ( wa kwanza kulia) asikiliza maelezo ya mtaalamu wa Kampuni ya Uhandisi ya MotaEngil Afrika - Tanzania ya ujenzi wa reli ya kisasa (standard gauge) eneo la Ngerengere kutoka kwa Mpima ardhi wa Kampuni hiyo , Juma Sospeter , wakati wa ziara yake na wajumbe wa kamati ya ulinzi na salama ya mkoa na wilaya ya Morogoro alipotembelea eneo la ujenzi wa kambi ya kampuni hiyo na njia ya reli ya kisasa ya “SGR “ katika kata ya Ngerengere , wilayani humo.
Mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dk Kebwe Stephen Kebwe ( wa pili kulia) asikiliza maelezo ya mtaalamu wa Kampuni ya Uhandisi ya MotaEngil Afrika - Tanzania ya ujenzi wa reli ya kisasa (standard gauge) ambaye ni Mpima ardhi , Juma Sospeter , wakati wa ziara yake na wajumbe wa kamati ya ulinzi na salama ya mkoa na wilaya ya Morogoro alipotembelea eneo la ujenzi wa kambi ya kampuni hiyo na njia ya reli ya kisasa ya “SGR “ eneo la kata ya Ngerengere , na ( kutoka kushoto) ni mkuu wa wilaya ya Morogoro, Regina Chonjo akizungumza jambo na Mhandisi mwendeshaji wa kampuni hiyo , Filipe Ataide. ( Picha na John Nditi).
Baadhi ya wataalamu wa Kitanzania wa Kampuni ya Uhandisi ya MotaEngil Afrika - Tanzania ya ujenzi wa reli ya kisasa (standard gauge) wakiendelea na kazi zao za hatua ya awali ya ujenzi huo eneo la Ngerengere wakati wa ziara ya mkuu wa mkoa wa Morogoro, Dk Kebwe Stephen Kebwe na wajumbe wa kamati ya ulinzi na salama ya mkoa na wilaya ya Morogoro walipotembelea eneo la ujenzi wa kambi ya kampuni hiyo na njia ya reli ya kisasa , “SGR “ katika kata ya Ngerengere , wilayani humo.

Na John Nditi, Morogoro

MKUU wa mkoa wa Morogoro, Dk Kebwe Stephen Kebwe ameitaka Kampuni ya Uhandisi ya MotaEngil Afrika  - Tanzania  ya ujenzi wa reli ya kisasa (standard gauge) kuhakikisha inawatumia wafanyakazi wa kitanzania waliopo katika  maeneo ya ujenzi wa mradi kwenye  ajira zisizo hitaji utaalamu zaidi. Dk Kebwe  alisema hayo alipokuwa na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa  na wilaya ya Morogoro  wakati alipotembelea eneo la ujenzi wa kambi  ya kampuni hiyo  na njia ya reli ya kisasa  inayotarajiwa  kujengwa ,kata ya Ngerengere , wilayani humo.

Mkuu huyo wa mkoa alisema , suala la ajira katika miradi kama hiyo mara nyingi limeleta  tatizo kubwa , lakini  kutokana na maelezo ya uongozi wa Kampuni pamoja na wa Serikali za kijiji na Kata ya Ngerengere kuwa upo utaratibu mzuri wa kushirikisha viongozi hao kuwapata wafanyakazi kwenye kazi zisizo na utaalamu.

 “ Hatuja pata matatizo na   wanaendelea vyema na kukamilishaji wa ujenzi wa kambi na kuanza njia ya reli ya SGR “ alisema Dk Kebwe .

Pamoja na hayo aliitaka Kampuni hiyo kuweka kipaumbele cha ajira  kwa  wakazi wa maeneo ya mradi na si  kuchukua  watu wa mbali ,  na kwamba kutokana na utaratibu uliowekwa kwa kushirikisha viongozi wa serikali za vijiji na kata utaondoa  malalamiko na hiyo  ni miongoni mwa sera ya kampuni. Mkuu huyo wa mkoa , aliitaka kampuni hiyo kutekeleza majukumu yake ya ujenzi wa reli ya kisasa kama mkataba ulivyo  na kwa kuzingatia kauli ya Rais  Dk John Magufuli wakati wa uzinduzi  wa ujenzi wa mradi huo ya kuwapata kukamil;ishaji uwe ndani ya miezi 24.

Pia  aliwataka  viongozi wa vijiji  na kata vilivyopo jirani na eneo  hilo   kushirikiana na wananchi ili kuhakikisha mradi huo unalindwa kwa lengo la kumwezesha mkandarasi kumaliza kwa wakati.

“ Wale wezi wa mafuta , vipiri na vitu vingine vya mradi huu washughulikiwe kikamilifu wanaponainika “ aliangiza Dk Kebwe kwa viongozi wa Serikali za vijiji vya kata ya Ngerengere.

Kwa upande wao ,Mpima ardhi  wa Kampuni hiyo , Juma Sospeter  pamoja na msimamizi wa maeneo ya ujenzi wa kambi hiyo Erick Mtasiwa ka nyakati tofauti wakitoa maelezo  kwa niaba ya kampuni, walisema zaidi ya vijana 50 kutoka vijiji vya tarafa ya Ngerengere, wamenufaika na ajira za mkataba za  kufanya kazi mbaimbali. Walisema ,  kampuni imezingatia maelekezo na miongozo inayotolewa na serikali kuyataka makampuni yanayo fanyashughuli mbalimbali ikiwemo ujenzi kuhakikisha inawatumia wafanyakazi wa kitanzania hususani katika ajira zisizo hitaji utaalam zaidi.

Awali, Mhandisi mwendeshaji wa kampuni ya MotaEngil  Afrika - Tanzania  ,  Filipe Ataide alisema  mpaka sasa hakuna changamoto yoyote iliyojitokeza na wamepenga  kukamilisha mradi huo kuzingatia makubaliano yaliyomo ndani ya mkataba na kwa ushauri wa Rais. Ujenzi wa reli ya kisasa (standard gauge) kwa  awamu  kuanzia Dar es Salaam hadi Morogoro  inatarajiwa kukamilika Oktoba 2019, ikiwa na urefu wa kilometa 300 na steshani sita  na inajengwa na Kampuni ya Uhansisi ya Mota-Engil  Afrika – Tanzania.


Hivyo makala VIJANA WA MOROGORO WANUFAIKA NA AJIRA UJENZI RELI MWENDO KASI ‘SGR’

yaani makala yote VIJANA WA MOROGORO WANUFAIKA NA AJIRA UJENZI RELI MWENDO KASI ‘SGR’ Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala VIJANA WA MOROGORO WANUFAIKA NA AJIRA UJENZI RELI MWENDO KASI ‘SGR’ mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/02/vijana-wa-morogoro-wanufaika-na-ajira.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "VIJANA WA MOROGORO WANUFAIKA NA AJIRA UJENZI RELI MWENDO KASI ‘SGR’"

Post a Comment