TAA YAPEWA WIKI 2 KUKUSANYA MADENI YOTE

TAA YAPEWA WIKI 2 KUKUSANYA MADENI YOTE - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa TAA YAPEWA WIKI 2 KUKUSANYA MADENI YOTE, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : TAA YAPEWA WIKI 2 KUKUSANYA MADENI YOTE
kiungo : TAA YAPEWA WIKI 2 KUKUSANYA MADENI YOTE

soma pia


TAA YAPEWA WIKI 2 KUKUSANYA MADENI YOTE




Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, akisisitiza 
jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari, kuhusu mipango ya 
Serikali ya kuendeleza kiwanja cha Ndege Mwanza kwa kuiboresha 
miundombinu ili kiwanja hicho kiwe cha Kimataifa, wakati alipokagua 
maendeleo ya upanuzi wa kiwanja hicho. 



  


Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa ametoa wiki 
mbili kwa Mamlaka ya Viwanja Ndege Nchini (TAA), kukusanya fedha za 
madeni ambayo inadai kutoka kwa watoa huduma mbalimbali katika viwanja 
vyote vya ndege ili ziweze kutumika kuendeleza miundombinu.

Kauli
hiyo ametoa jijini Mwanza, baada kukagua maendeleo ya upanuzi wa 
kiwanja cha ndege na hali ya uendeshaji katika kiwanja hicho ambapo 
amebaini kuwa kuna madeni ambayo yanaweza kulipika na kuweza kurahisisha
shughuli za kiuendeshaji ikiwemo kujenga uzio ili kuongeza usalama 
kiwanjani hapo.

"Nataka TAA mkusanye madeni yote mnayodai, fedha 
hizi zikipatikana zinaweza kutumika kujenga uzio kwa ajili ya kulinda 
usalama wa uwanja ili wananchi wasiweze kuvamia na pia usalama wa ndege 
zinazoruka na kutua", amesisitiza Prof. Mbarawa.


Amefafanua
kuwa kama Taasisi hizi zikikusanya madeni na watoa huduma wakalipa kodi
kwa wakati kutasaida Serikali kuboresha maendeleo ya miundombinu.

Kuhusu
maendeleo ya upanuzi wa kiwanja hicho. Prof. Mbarawa amesema 
ameridhishwa na kasi ya ujenzi ambapo kwa sasa umefikia asilimia 60.

Ameongeza kuwa ujenzi huo unategemewa kumalizika mwezi Julai mwaka huu na utagharimu kiasi cha shilingi takribani bilioni 94.

Aidha amesema Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo la abiria mara miradi inayoendelea kukamilika.


Naye
Msimamizi wa Kiwanja hicho ambaye ni Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara
(TANROADS), mkoa wa Mwanza, Mhandisi Joseph Mwami,  amesema kazi 
zinazoendelea kwa sasa ni pamoja na ujenzi wa jengo la kuongoza ndege, 
eneo la maegesho na njia za kuruka na kutua ndege 

Mhandisi 
Mwami, amefafanua kuwa njia ya kuruka na kutua ndege katika kiwanja 
hicho imeongezwa urefu wa mita 500 ili kuifanya kufikia urefu wa KM 3.5 
ili kuwezesha ndege kubwa za kimataifa kuweza kutua na kuruka katika 
kiwanja hicho.


Hivyo makala TAA YAPEWA WIKI 2 KUKUSANYA MADENI YOTE

yaani makala yote TAA YAPEWA WIKI 2 KUKUSANYA MADENI YOTE Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala TAA YAPEWA WIKI 2 KUKUSANYA MADENI YOTE mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/02/taa-yapewa-wiki-2-kukusanya-madeni-yote.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "TAA YAPEWA WIKI 2 KUKUSANYA MADENI YOTE"

Post a Comment