title : DKT. NDUGULILE ASHIRIKI UJENZI WA SHULE KATIKA ZOEZI LA KUAMSHA ARI YA WANANCHI KUFANYA SHUGHULI ZA MAENDELEO WILAYANI KISARAWE
kiungo : DKT. NDUGULILE ASHIRIKI UJENZI WA SHULE KATIKA ZOEZI LA KUAMSHA ARI YA WANANCHI KUFANYA SHUGHULI ZA MAENDELEO WILAYANI KISARAWE
DKT. NDUGULILE ASHIRIKI UJENZI WA SHULE KATIKA ZOEZI LA KUAMSHA ARI YA WANANCHI KUFANYA SHUGHULI ZA MAENDELEO WILAYANI KISARAWE
Na Kitengo cha Mawailiano WAMJW
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Dkt Faustine Ndugulile ameshiriki kazi ya ujenzi wa shule ya msingi Chambasi Wilayani Kisarawe ikiwa ni zoezi la kuamsha ari ya wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo katika maeneo yao.
Akizungumza wakati wa zoezi hilo Dk. Ndugulile amesema kuwa kwa kipindi kirefu dhana ya wananchi kujitolea katika kufanya kazi za maendeleo imepungua kwa kiasi kikubwa na kuiachia Serikali ikitoa kila kitu kutekeleza miradi ya maendeleo hata kama inawezekana kazi hizo kutekelezwa na wananchi.
Dkt. Ndugulile ameongeza kuwa kwa kipindi cha sasa cha Serikali ya Awamu ya Tano ya Hapa kazi tu wananchi hawana budi kujitoa katika kufanya shughuli za maendeleo katika maeneno hayo ili kuisaidia Serikali na kujisaidia wao wenyewe kujiletea maendeleo.
“Msisubiri kila kitu kifanywe na Serikali vingine mnaweza kufanya weneyewe hongereni sana ninyi ni mfano wa kuigwa kwa vijiji vingine katika hili” alisema Dkt. Ndugulile.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Dkt Faustine Ndugulile akishiriki kuchanganya mchanga wa kutengeneza zege kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Msingi Chambasi wakati wa zoezi la kuamsha ari ya wananchi katika kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo yao katika wilaya ya Kisarawe.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Dkt Faustine Ndugulile akishiriki kutengeneza tofali wakati wa zoezi la kuamsha ari ya wananchi katika kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo yao aliposhiriki katika ujenzi wa shule ya Msingi Chambasi wilayani Kisarawe.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Dkt Faustine Ndugulile akishiriki kubeba ndoo ya zege wakati wa zoezi la kuamsha ari ya wananchi kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo yao aliposhiriki katika ujenzi wa shule ya Msingi Chambasi wilayani Kisarawe.
Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto Bibi.Sihaba Nkinga akishiriki kubeba ndoo ya zege wakati wa zoezi la kuamsha ari ya wananchi katika kufanya shughuli za maendeleo katika maeneo yao aliposhiriki katika ujenzi wa shule ya Msingi Chambasi wilayani Kisarawe.
Hivyo makala DKT. NDUGULILE ASHIRIKI UJENZI WA SHULE KATIKA ZOEZI LA KUAMSHA ARI YA WANANCHI KUFANYA SHUGHULI ZA MAENDELEO WILAYANI KISARAWE
yaani makala yote DKT. NDUGULILE ASHIRIKI UJENZI WA SHULE KATIKA ZOEZI LA KUAMSHA ARI YA WANANCHI KUFANYA SHUGHULI ZA MAENDELEO WILAYANI KISARAWE Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala DKT. NDUGULILE ASHIRIKI UJENZI WA SHULE KATIKA ZOEZI LA KUAMSHA ARI YA WANANCHI KUFANYA SHUGHULI ZA MAENDELEO WILAYANI KISARAWE mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/12/dkt-ndugulile-ashiriki-ujenzi-wa-shule.html
0 Response to "DKT. NDUGULILE ASHIRIKI UJENZI WA SHULE KATIKA ZOEZI LA KUAMSHA ARI YA WANANCHI KUFANYA SHUGHULI ZA MAENDELEO WILAYANI KISARAWE"
Post a Comment