title : Serikali kuajiri maafisa ugani 1,487 mwaka wa fedha 2017/2018
kiungo : Serikali kuajiri maafisa ugani 1,487 mwaka wa fedha 2017/2018
Serikali kuajiri maafisa ugani 1,487 mwaka wa fedha 2017/2018
Serikali imepanga kuajiri maafisa Ugani 1,487 katika mwaka wa Fedha 2017/2018 ili kuziba pengo la upungufu wa wataalamu hao kote nchini na kuongeza tija katika uzalishaji kwenye sekta ya Kilimo.
Akijibu swali la Mbunge wa Nanyamba Mhe. Abdalla Chikota wakati wa Kipindi cha maswali na majibu Bungeni, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika amesema kuwa kati ya mwaka 2013/2014 hadi 2016/2017 jumla ya Maafisa Ugani 5,710 waliajiriwa katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa.
“Serikali imekuwa ikitoa vibali vya ajira za Maafisa Ugani katika Mamlaka za Serikali ya Mitaa kila mwaka wa fedha kutegemea uwezo wa bajeti,” alisisitiza Mkuchika.
Akisisitiza Mhe. Mkuchika amesema kuwa Serikali inatambua upungufu wa Maafisa Ugani hasa katika Halmashauri mpya na Miji na itahakikisha inawapeleka Maafisa hao ili kuleta uwiano kati ya Halmashuri Kongwe na zile mpya.
Aliongeza kuwa Wizara yake itashirikiana na Wizara ya Kilimo kuhakikisha kuwa udahili katika vyuo vya Ugani unaongezeka ili idadi ya wataalamu hao iongezeka kulingana na mahitaji.
Katika Kukuza na kuongeza tija Katika Sekta ya Kilimo Serikali imeweka mkazo katika kuongeza ujuzi na maarifa ya Wataalam wa Kilimo ili kuendana na dhana ya ujenzi wa uchumi wa Viwanda.
Na Frank Mvungi- Maelezo, Dodoma
Hivyo makala Serikali kuajiri maafisa ugani 1,487 mwaka wa fedha 2017/2018
yaani makala yote Serikali kuajiri maafisa ugani 1,487 mwaka wa fedha 2017/2018 Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Serikali kuajiri maafisa ugani 1,487 mwaka wa fedha 2017/2018 mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/11/serikali-kuajiri-maafisa-ugani-1487.html
0 Response to "Serikali kuajiri maafisa ugani 1,487 mwaka wa fedha 2017/2018"
Post a Comment