TCRA Yawaasa Wamiliki Wa Mitandao Ya Kijamii Kuchuja Habari Zao Kwa Weredi

TCRA Yawaasa Wamiliki Wa Mitandao Ya Kijamii Kuchuja Habari Zao Kwa Weredi - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa TCRA Yawaasa Wamiliki Wa Mitandao Ya Kijamii Kuchuja Habari Zao Kwa Weredi, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : TCRA Yawaasa Wamiliki Wa Mitandao Ya Kijamii Kuchuja Habari Zao Kwa Weredi
kiungo : TCRA Yawaasa Wamiliki Wa Mitandao Ya Kijamii Kuchuja Habari Zao Kwa Weredi

soma pia


TCRA Yawaasa Wamiliki Wa Mitandao Ya Kijamii Kuchuja Habari Zao Kwa Weredi

Wamiliki wa mitandao ya kijamii wameaswa kuchuja habari zao ambazo wamekuwa wakizipata na kuzisambaza kwa jamii kwa njia mbalimbali ikiwemo kwa Redio ama televisheni za Mitandaoni.
 
Hayo ameyasema leo Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui , Valerie Msoka wakati alipokutana wamiliki wa mitandao ya Kijamii pamoja na waandishi wa habari.

Valerie amesema kuwa upashanaji wa habari lazima kuangalia na usalama wa nchi pamoja kuacha uchochezi ambao unachonganisha  jamii au mamlaka.

Amesema kuwa takribani miaka mitano kulikuwa hakuna fursa za kupata matangazo ya televisheni kupitia mitandao ya kijamii, lakini sasa imeenea kwa watanzania wengi na inaendelea kuongezeka kadri ya teknolojia inavyokuwa, hivyo kunahitajika kuwepo umuhimu wa kusimamia huduma ya mitandao hiyo ili iweze kuleta tija kwenye taifa na si vinginevyo.

Valerie amesema kuwa TCRA kupitia kamati ya maudhui inatambua na kuthamini kuwepo kwa fursa ya upashanaji wa habari na serikali iliamua kuruhusu huduma hiyo wakati miongozo na taratibu stahiki zikiendelea kutayarishwa.

Amesema vyombo vya habari katika mitandao ya kijamii vya Radio, Televisheni na bado teknolojia inaendelea kukua na haviwezi kuzuia kutokana na mfumo wa upashanaji wa habari. 

Mwenyekiti huyo anasema habari zingine hazina tija kwa jamii na zingine zinaleta uchochezi ndani ya jamii na wakati mwingine kuingilia faragha za watu ambazo hazitakiwa kufikia jamii kama sehemu ya habari.

Amesema wadau wa mitandao ya kijami na watumiaji wa mitandao hiyo wanahakikisha wanahabarisha kwa kuzingatia habari zinazojenga umoja wa kitaifa, mshikamano na ushirikiano baina ya watanzania bila kujenga hofu, kuchochea chuki na uhasama baina ya watanzania. 

Aidha amesema habari za matusi katika mitandao ya kijamii hayavumiliki ,kwani zinakiuka misingi ya uandishi na uhuru na wajibu wake.


Hivyo makala TCRA Yawaasa Wamiliki Wa Mitandao Ya Kijamii Kuchuja Habari Zao Kwa Weredi

yaani makala yote TCRA Yawaasa Wamiliki Wa Mitandao Ya Kijamii Kuchuja Habari Zao Kwa Weredi Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala TCRA Yawaasa Wamiliki Wa Mitandao Ya Kijamii Kuchuja Habari Zao Kwa Weredi mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/09/tcra-yawaasa-wamiliki-wa-mitandao-ya_13.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "TCRA Yawaasa Wamiliki Wa Mitandao Ya Kijamii Kuchuja Habari Zao Kwa Weredi"

Post a Comment