MBUNGE CHALINZE AKEMEA UFUGAJI HOLELA AMBAO UHARIBU RUTUBA

MBUNGE CHALINZE AKEMEA UFUGAJI HOLELA AMBAO UHARIBU RUTUBA - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa MBUNGE CHALINZE AKEMEA UFUGAJI HOLELA AMBAO UHARIBU RUTUBA, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : MBUNGE CHALINZE AKEMEA UFUGAJI HOLELA AMBAO UHARIBU RUTUBA
kiungo : MBUNGE CHALINZE AKEMEA UFUGAJI HOLELA AMBAO UHARIBU RUTUBA

soma pia


MBUNGE CHALINZE AKEMEA UFUGAJI HOLELA AMBAO UHARIBU RUTUBA

Na Mwamvua Mwinyi, Chalinze

MBUNGE wa jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete, amekabidhi pikipiki kumi, zilizogharimu sh. Mil. 22.5 kwa maafisa mifugo wa kata, ili waweze kuwafikia wafugaji wote, kupeleka sera ya kufuga kisasa na kuondoa migogoro na wakulima. Aidha amekemea tabia inayofanywa na baadhi ya wafugaji ya kufuga kizamani kwa kuswaga makundi ya ng’ombe kwenye eneo moja hali inayosababisha kuharibu rutuba.

Akikabidhi pikipiki hizo, huko Lugoba Ridhiwani alieleza, vyombo hivyo vya usafiri vikatumike kusimamia majukumu waliyonayo badala ya kuvitumia kwa matumizi yao binafsi. Aliwataka jamii ya wafugaji kuachana na mtazamo hasi wa kufuga kizamani mifugo lundo isiyo na tija pamoja na kuingia katika maeneo ambayo hayajatengwa kwa ajili yao.

Ridhiwani, alieleza kuwa wafugaji hasa wa kimasai wanaamini kuwa na ng’ombe wengi ndio utajiri, waondoe dhana hiyo kwani sio sifa, wajaribu kufuga mifugo michache na kujiwekea kasumba ya kufuga kwenye mazizi. Hata hivyo, alimpongeza mkurugenzi wa halmashauri ya Chalinze, Edes Lukoa kwa kusimamia na kuyafanyia kazi maazimio ya madiwani ambayo huwa wakitoa.

Ridhiwani, alito mafuta  lita tano kwa kila pikipiki na kuahidi kuangalia uwezekano wa kufanya utaratibu kila mwezi kwenye posho zinazokwenda katika kata maafisa mifugo hao wataongeza japo 5,000 kwa ajili ya mafuta ya pikipiki hizo.

Kwa upande wake mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Lukoa alisema pikipiki hizo zimenunuliwa kutokana na mapato ya ndani ya halmashauri. Alizitaja kata zilizokabidhiwa usafiri huo kuwa ni sanjali na Vigwaza, Kibindu, Mbwewe, Talawanda, Msata, Kimange, Kiwangwa, Miono, Ubena Zomozi na Mandela.
Mbunge wa jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete akifurahi jambo na baadhi ya watendandaji wakati wa zoezi la kukabidhi pikipiki hizo.

Lukoa  alieleza kwa msimu wa bajeti 2017/2018 wanatarajia kununua pikipiki nyingine 15 kwa ajili ya watendaji na nyingine nane kwa ajili ya maafisa mifugo wa kata na vijiji. Aliwashukuru madiwani kwa ushirikiano na CMT kwa mchango  wao mkubwa katika kutoa maazimio yaliyotakiwa yatekelezwe na halmashauri na sasa yamefanikiwa. 

SOMA ZAIDI HAPA


Hivyo makala MBUNGE CHALINZE AKEMEA UFUGAJI HOLELA AMBAO UHARIBU RUTUBA

yaani makala yote MBUNGE CHALINZE AKEMEA UFUGAJI HOLELA AMBAO UHARIBU RUTUBA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala MBUNGE CHALINZE AKEMEA UFUGAJI HOLELA AMBAO UHARIBU RUTUBA mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/08/mbunge-chalinze-akemea-ufugaji-holela.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "MBUNGE CHALINZE AKEMEA UFUGAJI HOLELA AMBAO UHARIBU RUTUBA"

Post a Comment