title : WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO YASHIRIKI KIKAMILIFU MAONESHO YA SABASABA
kiungo : WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO YASHIRIKI KIKAMILIFU MAONESHO YA SABASABA
WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO YASHIRIKI KIKAMILIFU MAONESHO YA SABASABA
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC), Samwel Kamanga akiweka saini katika kitabu chwa wageni alipotembelea Banda la Wizara ya Fedha na Mipango katika Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara (Saba saba) yanayoendelea katika viwanja vya JK Nyerere barabara ya Kilwa, Jijini Dar es salaam. Kulia ni Afisa Habari wa Wizara ya Fedha na Mipango Josephine Majura.

Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Sabasaba Moshingi akisaini kitabu cha wageni katika banda la GEPF wakati alipotembelea banda hilo katika Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara (Saba saba) yanayoendelea katika viwanja vya JK Nyerere barabara ya Kilwa, Jijini Dar es salaam
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage (kulia) akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Masoko Shirika la Bima la Taifa Bw. Elisante Maleko wakati alipotembelea Taasisi hiyo iliyopo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango katika banda la Wizara hiyo katika Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara (Saba saba) yanayoendelea katika viwanja vya JK Nyerere barabara ya Kilwa, Jijini Dar es salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dorothy Mwanyika (kushoto) akipokea kitabu kutoka Taasisi ya Uhasibu Arusha (T) (IAA) alipotembelea banda la Wizara ya Fedha na Mipango katika Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara (Saba saba) yanayoendelea katika viwanja vya JK Nyerere barabara ya Kilwa, Jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw. William Erio (katikati) akizungumza na Jumanne Nyamgunda Afisa Mwandamizi wa Bima wakati alipotembelea Shirika la Bima la Taifa katika Banda la Wizara ya Fedha na Mipango lililopo katika viwanja vya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa (Saba saba) jijini Dar es Salaam ambapo aliwapongeza kwa huduma nzuri, kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Benny Mwaipaja na kulia ni Mwanaidi Shemweta Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano NIC.
Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Sabasaba Moshingi akisaini kitabu cha wageni katika banda la GEPF wakati alipotembelea banda hilo katika Maonesho ya 41 ya Kimataifa ya Biashara (Saba saba) yanayoendelea katika viwanja vya JK Nyerere barabara ya Kilwa, Jijini Dar es salaam
Hivyo makala WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO YASHIRIKI KIKAMILIFU MAONESHO YA SABASABA
yaani makala yote WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO YASHIRIKI KIKAMILIFU MAONESHO YA SABASABA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO YASHIRIKI KIKAMILIFU MAONESHO YA SABASABA mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/07/wizara-ya-fedha-na-mipango-yashiriki.html
0 Response to "WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO YASHIRIKI KIKAMILIFU MAONESHO YA SABASABA"
Post a Comment