Balozi Seif Ali Iddi akutana na Rais wa Taasisi ya Ushauri wa masuala ya Uhandisi ya Endsight

Balozi Seif Ali Iddi akutana na Rais wa Taasisi ya Ushauri wa masuala ya Uhandisi ya Endsight - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Balozi Seif Ali Iddi akutana na Rais wa Taasisi ya Ushauri wa masuala ya Uhandisi ya Endsight, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Balozi Seif Ali Iddi akutana na Rais wa Taasisi ya Ushauri wa masuala ya Uhandisi ya Endsight
kiungo : Balozi Seif Ali Iddi akutana na Rais wa Taasisi ya Ushauri wa masuala ya Uhandisi ya Endsight

soma pia


Balozi Seif Ali Iddi akutana na Rais wa Taasisi ya Ushauri wa masuala ya Uhandisi ya Endsight

Taasisi ya Ushauri wa masuala ya Uhandisi ya Endsight iliyo chini ya usimamizi wa Shirika la Changamoto ya Millenia la Marekani (MCC) imeazimia kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kuimarisha miradi ya Maendeleo kupitia miundombinu ya Mawasiliano na huduma za Kijamii. 
Rais wa Taasisi hiyo Bwana Matthew McLean alitoa kauli hiyo wakati alipofanya mazungumzo na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Vuga Mjini Zanzibar. 
Mazungumzo hayo pia yalijumuisha Waziri wa Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira Mh. Salama Aboud Talib, Naibu Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usarifishaji Zanzibar Mh. Mohamed Ahmed Salum pamoja na watendaji wakuu wa baadhi ya Taasisi za Serikali. 
Bwana Matthew alisema Endsight imekuwa ikitoa ushauri wa Kitaalamu katika fani ya uhandisi katika kuona kiwango cha miundombinu kinachowekwa kwenye miradi inayohusika zaidi na masuala ya uhandisi inatekelezwa katika hadhi na daraja inayotakiwa kitaalamu. Alisema miundombinu ya bara bara na Mawasiliano, kilimo ikiwemo pia miradi ya huduma za maji safi na salama inahitaji ungalizi sahihi katika uanzishwaji wake ili wakati inapoanza kufanya kazi itoe huduma sahihi iliyokusudiwa kitaalamu. 
Naye Waziri wa Ardhi, Maji, Nishati na Mazingira Mh. Salama Aboud Talib pamoja na watendaji wa Serikali walimueleza Bwana Matthew kwamba Zanzibar bado inakabiliwa na changamoto wa upatikanaji wa maji safi na salama katika baadhi ya maeneo.
  Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Vuga Mjini Zanzibar akizungumza na Rais wa Taasisi ya Ushauri wa masuala ya Uhandisi  ya Endsight  iliyo chini ya usimamizi wa Shirika la Changamoto ya Milenia la Marekani (MCC)  Bwana Matthew McLean ofisini kwake Vuga mjini Zanzibar 
Balozi Seif Ali Iddi Kati kati akiwa katika pamoja na Rais wa Taasisi ya Ushauri wa masuala ya Uhandisi  ya Endsight  Bwana Matthew  McLean aliyeko upande wa Kulia yake , Waziri Ardhi Mh. Salama Aboud Talib Kushoto  yake, Naibu Waziri Ujenzi Mh. Mohamed Ahmed Salum wa Pili kutoka Kushoto pamoja na baadhi ya Watendaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Picha na – OMPR – ZNZ. 


Hivyo makala Balozi Seif Ali Iddi akutana na Rais wa Taasisi ya Ushauri wa masuala ya Uhandisi ya Endsight

yaani makala yote Balozi Seif Ali Iddi akutana na Rais wa Taasisi ya Ushauri wa masuala ya Uhandisi ya Endsight Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Balozi Seif Ali Iddi akutana na Rais wa Taasisi ya Ushauri wa masuala ya Uhandisi ya Endsight mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/07/balozi-seif-ali-iddi-akutana-na-rais-wa.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Balozi Seif Ali Iddi akutana na Rais wa Taasisi ya Ushauri wa masuala ya Uhandisi ya Endsight"

Post a Comment