title : WADAU WA ELIMU WILAYA YA KILWA WAJENGEWA UWEZO KUHAMASISHA UKUSANYAJI WA RASILIMALI ZA NDANI KUBORESHA SEKTA YA ELIMU
kiungo : WADAU WA ELIMU WILAYA YA KILWA WAJENGEWA UWEZO KUHAMASISHA UKUSANYAJI WA RASILIMALI ZA NDANI KUBORESHA SEKTA YA ELIMU
WADAU WA ELIMU WILAYA YA KILWA WAJENGEWA UWEZO KUHAMASISHA UKUSANYAJI WA RASILIMALI ZA NDANI KUBORESHA SEKTA YA ELIMU
Katika kuzitafutia ufumbuzi changamoto za utoaji wa elimu bora hapa nchini leo Mtandao wa Elimu Tanzania (TENMET) wakishirikiana na ActionAid Tanzania wameandaa mkutano uliowakutanisha wanachama wa chama cha walimu Tanzania (CWT/TTU) na wadau wa elimu katika mkoa wa Lindi wilaya ya Kilwa kwa siku tatu ili kupanga mpango kazi wa utetezi na ushawishi wa masuala ya elimu yatakayoleta matokeo chanya kwenye masuala ya elimu hapa nchini.
Mkutano huu ulikuwa ulingazia changamoto zinazoikabili elimu ya msingi hapa nchini ikiwemo upungufu wa vyumba vya madarasa, upungufu wa ofisi za walimu, upungufu wa vyoo vya wanafunzi, uwiano usiokubalika kitaratibu wa mwalimu na wanafunzi, shule nyingine kukosa kabisa mwalimu wa kike, upungufu wa nyumba za walimu, kutokutosha kwa fedha za ruzuku, utegemezi wa bajeti ya nchi unaoathiri pia bajeti ya elimu na kusababisha Serikali kushindwa kugharimia kiufanisi utoaji wa elimu.
Mgawanyo wa ruzuku usiozingatia mahitaji ya wenye uhitaji maalumu, jinsia na mahitaji ya kijiografia na pia shule changa na zile ambazo ni kongwe. Kuwa na mipango ya kibaguzi kwa shule inayofanya vizuri ndiyo inapewa fedha (payment for results- P4R) kutoka mpango wa BRN bila kujali mizania ya usawa wa mazingira kati ya shule na shule. Kukosekana kwa mafunzo kazini kwa walimu, kutopandishwa madaraja walimu na utolipwa kwa wakati stahiki za walimu wanaohamishwa/kustaafu mfano pesa ya usafiri.
Katika majadiliano washiriki walichangia juu Upotevu wa kodi nchini hususani katika sekta ya madini na viwanda ndio chanzo cha kukosa fedha za kutosha kugharimia sekta ya elimu nchini.
Afisa Mradi wa Elimu kutoka TENMET, Bi. Alistidia Kamugisha akifungua mafunzo ya siku tatu na kuelezea juu ya uhusiano wa ukusanyaji kodi na maendeleo katika sekta ya elimu nchini ili kutafuta ufumbuzi wa changamoto za utoaji wa elimu bora hapa nchini kwenye mkutano uliowakutanisha wanachama wa chama cha walimu Tanzania (CWT/TTU) na wadau wa elimu katika wilaya ya Kilwa mkoani Lindi.
Afisa kutoka ActionAid Tanzania, Joyce John akitoa mada kuhusu utetezi wa haki za watoto maashuleni kwenye mkutano uliowakutanisha wanachama wa chama cha walimu Tanzania (CWT/TTU) na wadau wa elimu katika wilaya ya Kilwa mkoani Lindi.
Mwalimu Khamis Kikwajuni akichangia mada kuhusu haki za watoto mashuleni pamoja na Umuhimu wa ukusanyaji wa mapato ya ndani kuwekeza katika sekta ya elimu kwenye mafunzo yaliyoandaliwa na TENMET wakishirikiana na ActionAid Tanzania.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Hivyo makala WADAU WA ELIMU WILAYA YA KILWA WAJENGEWA UWEZO KUHAMASISHA UKUSANYAJI WA RASILIMALI ZA NDANI KUBORESHA SEKTA YA ELIMU
yaani makala yote WADAU WA ELIMU WILAYA YA KILWA WAJENGEWA UWEZO KUHAMASISHA UKUSANYAJI WA RASILIMALI ZA NDANI KUBORESHA SEKTA YA ELIMU Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala WADAU WA ELIMU WILAYA YA KILWA WAJENGEWA UWEZO KUHAMASISHA UKUSANYAJI WA RASILIMALI ZA NDANI KUBORESHA SEKTA YA ELIMU mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/06/wadau-wa-elimu-wilaya-ya-kilwa.html
0 Response to "WADAU WA ELIMU WILAYA YA KILWA WAJENGEWA UWEZO KUHAMASISHA UKUSANYAJI WA RASILIMALI ZA NDANI KUBORESHA SEKTA YA ELIMU"
Post a Comment