Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki kukutana kesho Dar

Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki kukutana kesho Dar - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki kukutana kesho Dar, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki kukutana kesho Dar
kiungo : Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki kukutana kesho Dar

soma pia


Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki kukutana kesho Dar

Na Immaculate Makilika- MAELEZO 
WAKUU wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki wanatarajia kufanya mazungumzo ya pamoja baina yao katika Mkutano wa kawaida wa 18 utakaofanyika kesho Mei 20 katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam. 
 Mkutano huo unatarajiwa kupokea ripoti ya usuluhishi ya kamati inayoongozwa na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Benjamini William Mkapa kuhusu mgogoro wa nchini Burundi. Mambo mengine yatakayozungumzwa katika mkutano huo ni pamoja na taarifa na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa katika mkutano wa 17 wa Wakuu wa nchi za Jumuiya hiyo. 
 Masuala hayo ni pamoja na namna ya kuwezesha uundaji wa magari katika Jumuiya ya Afrika Mashariki na kupunguza uagizaji wa magari yaliyotumika kutoka nje ya Jumuiya, mapitio kuhusu sekta ya nguo na ngozi. 
 Aidha masuala mengine ni pamoja na kuzuia ama kuondoa uagizaji wa nguo na viatu vilivyotumika kutoka nje. 
 Wakuu hao wa Nchi pia wanatarajia kujadili namna endelevu ya uchangiaji wa bajeti ya Jumuiya hiyo kwa nchi wananchama. 
 Aidha, katika Mkutano huo wa 18 Tanzania itakabidhi nafasi ya mwenyekiti wa Jumuiya hiyo iliyoishika kwa muda wa miaka miwili kwa nchi ya Jamhuri ya Uganda.


Hivyo makala Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki kukutana kesho Dar

yaani makala yote Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki kukutana kesho Dar Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki kukutana kesho Dar mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/05/wakuu-wa-nchi-za-afrika-mashariki.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki kukutana kesho Dar"

Post a Comment