title : wananchi wa arumeru wahakikishiwa ulinzi muda wote
kiungo : wananchi wa arumeru wahakikishiwa ulinzi muda wote
wananchi wa arumeru wahakikishiwa ulinzi muda wote
Na Woinde Shizza, Michuzi TV Arusha
Mkuu Wa Wilaya Arumeru Jerry Muro amewakikishia wananchi wake ataendelea kutatua changamoto zinazo wakabili ikiwemo changamoto za ardhi.
Ameyasema hayo Leo wakati akimtambulisha kamanda Wa polisi mpya Wa mkoa Wa Arusha Jonathan Shana alipofanya ziara ya kutembelea halmashauri hiyo.
Alisema kuwa ofisi yake imeweka mkakati Wa kutatua kero za wananchi wake ambapo ofisi yake imeweka wanasheria wanne ambao watawasaidia wananchi wasio kuwa na uwezo .
"Kuna wananchi wengi ambao wana kesi mbalimbali na wanataka msaada Wa kisheria lakini wanashidwa kuweka wanasheria kutokuwa na uwezo hivyo nimeamua kuwatafutia wanasheria hawa wanne ambao nitawalipa Mimi mwenyewe kwa mshahara wangu Mdogo ninaopewa ili wafanye Kazi yakutatua matatizo ya wananchi yanaohusu sheria " alisema Muro.
Akiongea na wananchi kamanda Wa polisi mkoa Wa Arusha Jonathan Shana aliwakikishia wananchi Wa Wilaya ya Meru kuondoa askari yeyote atakiuka taratibu na kanuni za Kazi yao kwa kuchafua sifa za jeshi la polisi.
"Napenda kuwaahaidi wananchi kuwa sitamfumbia macho askari yeyote ambae atakiuka sheria ,na Mwananchi yeyote ambae utaona askari yeyote anaekiuka sheria chukua simu nipigie simu nimshughulikie na naahidi nitasimamia vyema na sitamvumbia maji" alisema kamanda
Wakati huo huo mkurugenzi Wa halmashaiuri ya Meru Mhe. Emanuel Mkongo alimuhakikishia kamanda Wa polisi Wa mkoa Wa Arusha ulinzi na Amani katika kipindi cha uchaguzi Wa ubunge Wa jimbo la Arumeru mashariki unaotarajiwa kufanyika mapema mei 19.
Alisema kuwa mpaka sasa jumla ya wagombea wa vyama 11 wamechukuwa fomu za kugombea na leo april 19 ndio mwisho Wa kurudisha fomu.
"Vyama hivyo vilivyochukuwa fomu NCCR mageuzi,CUF,ADA TADEA,Chama cha mapinduzi (CCM),AAFP,SAU,Demokrasia makini,DP pamoja na UPDP vyama vyote hivi vimesimamisha wagombea na wanatarajia kurudisha fomu Kesho" alisema Mkongo.
Uchaguzi huu unafanyika Mara baada ya mbunge Wa jimbo hilo kuvuliwa ubunge Joshua Nasari kutona na kutouzuria vikao vitatu vya Bunge bila kutona taarifa yoyote kwa spika Wa Bunge.
Kamanda Wa polisi mkoa Wa Arusha Afande Jonathan Shana akiongea na wananchi nje ya ofisi ya mkuu wa wilaya ya Arumeru Nhe. Jerry Muro wa kwanza kulia
Mkurugenzi Wa halmashauri ya Meru Mhe. Emmanuel Mkongoa kiongea na waandishi wa habari ofisini kwake
Hivyo makala wananchi wa arumeru wahakikishiwa ulinzi muda wote
yaani makala yote wananchi wa arumeru wahakikishiwa ulinzi muda wote Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala wananchi wa arumeru wahakikishiwa ulinzi muda wote mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2019/04/wananchi-wa-arumeru-wahakikishiwa.html
0 Response to "wananchi wa arumeru wahakikishiwa ulinzi muda wote"
Post a Comment