WANYAMA HIFADHI YA RUAHA WAFA KWA KUKOSA MAJI

WANYAMA HIFADHI YA RUAHA WAFA KWA KUKOSA MAJI - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa WANYAMA HIFADHI YA RUAHA WAFA KWA KUKOSA MAJI, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : WANYAMA HIFADHI YA RUAHA WAFA KWA KUKOSA MAJI
kiungo : WANYAMA HIFADHI YA RUAHA WAFA KWA KUKOSA MAJI

soma pia


WANYAMA HIFADHI YA RUAHA WAFA KWA KUKOSA MAJI

Na Francis Godwin, Iringa.

IMEELEZWA  kuwa  shughuli  za  kibinadamu  zikiwemo  za  kilimo  zinazofanywa  kando kando  ya  mto  Ruaha  mkuu  na  vyanzo  vya maji    katika mikoa ya Njombe ,Mbeya na  Iringa ambavyo  vinaelekeza maji yake  katika  mto  Ruaha  mkuu  ni  chanzo  cha mto  Ruaha  kuendelea  kukauka na  kusababisha  baadhi ya  wanyama  wanaotegemea  maji  kuanza kufa.

Akizungumza na  wanahabari  waliotembelea  hifadhi hiyo ya  Ruaha kwa ajili ya  kuhamasisha  jamii  ya  kitanzania   kujenga utamaduni wa  kufanya  utalii wa ndani katika hifadhi  hiyo ya Ruaha na vivutio  vingine  vya  utalii mikoa ya  nyanda  za  juu  kusini , mhifadhi  mkuu wa  hifadhi ya Ruaha Iringa Izumbe  Msindai alisema  kuwa  mbali ya  vifo  vya  wanyama  kuendelea  kuongezeka  ila magonjwa ya  mlipuko kwa wanyama  yamekuwa  yakiibuka mara kwa mara.

Msindai  alisema  kuwa  hali ya  kina cha maji  katika  mto   Ruaha  mkuu kimezidi  kupungua na  kwa  sasa maji yaliyopo  ni machache  sana  na   hivyo  kupelekea  baadhi ya wanyama  kuanza  kufa kwa  kukosa maji na wengine  kumbumbwana  mlipuko kwa magonjwa mbali mbali .

 Alisema  miaka ya  nyuma   kipindi kama   hiki mto Ruaha mkuu ulikuwa  unatiririsha  maji kwa kipindi cha mwaka mzima pasipo maji  kupunguka  ila kwa  miaka ya   hivi karibuni  hadi mwaka huu maji yamekuwa yakikata mapema  zaidi na  kupelekea  wanyama  kufa kwa  kukosa maji .

"  Zimekuwepo  jitihada mbali mbali za  serikali katika  kukabiliana na uharibifu wa vyanzo  vya maji  vinavyoelekeza maji yake katika mto Ruaha na  jitihada  hizo zimeendelea  kuzaa matunda  ila bado jamii inapaswa  kuelimishwa  zaidi juu ya matumizi   sahihi ya maji " alisema 

Kwa  upande  wao kama hifadhi  ya Rauha  wamepata  kutembelea  vyanzo mbali mbali  vya maji kama kile cha Kimani wilayani Makete mkoani Njombe na kuona maji yakiendelea  kutiririka kwa  wingi ila  sababu ya  maji kutofika katika mto Ruaha  inawezekana  maji hayo yanaishia  njiani .

katika hatua nyingine  Msindai  aliwataka  wanahabari  nchini  kuwa kielelezo  chema katika Taifa kwa kuendelea  kuhamasisha  jamii  kuepuka uharibifu  wa mazingira  pamoja na  kuwahamasisha watanzania  kutembelea   hifadhi  hiyo ya  Ruaha  kujifunza utali  wa ndani  badala ya  kuwaachia  wageni  kutoka nje .

Alisema kuwekuwa na tofauti kubwa ya gharama za kiingilio  katika  hifadhi  kati ya  watalii wa ndani na watalii wa  kigeni na  kuwa serikali  kupitia   wizara  husika  imefanya  hivyo  ili  kila mtanzania kuweza  kutembelea  hifadhi  bila kikwazo chochote na kuwa  serikali imeendelea  kuboresha  miundo mbinu ya  kufika  hifadhini hapo kirahisi zaidi .

Mhadhiri  wa  chuo  kikuu cha Iringa   Jimson Sanga ambe ni mratibu wa  mradi wa  kuendeleza  utamaduni na utalii nyanda za juu  kusini alipongeza  jitihada za  hifadhi ya  Ruaha  Iringa kwa  kuendelea  kutumia  mbinu mbali mbali  za kuitangaza hifadhi  hiyo  kwani  alisema   pamoja na kuwa  hifadhi ya  Ruaha  ni kubwa  kuliko  zote Afrika ila kwa Tanzania nguvu za utalii  zilielekezwa  hifadhi  za kaskazini ila  sasa  serikali imepania  kuelekeza   nguvu zake katika hifadhi za  kusini ikiwemo ya Ruaha Iringa .

Sanga alisema  iwapo  vyombo  vya habari vitaendelea na kasi ya  kueleza uzuri wa  hifadhi za kusini ni  wazi Taifa linaweza kuongeza mapato  yake  kutokana na sekta hiyo ya utalii  pekee .

 Tembo  wa  hifadhi ya  Ruaha  mkoani Iringa wakihangaika kutafuta  maji katika  vidimbwi  kufuatia kukauka kwa mto Ruaha mkuu  kutokana na uendeshaji  wa shughuli za kibinadamu kando kando ya mto Ruaha kwa mikoa ya Iringa , Mbeya na Njombe (PICHA NA  FRANCIS GODWIN).
Baadhi ya wanahabari kutoka mkoa wa Iringa na Morogoro wakiwapiga picha wanyama aina ya Pundamilia waliokuwa wakijipatia malisho yao ndani ya hifadhi ya Taifa ya Ruaha Iringa ,waandishi hao walikuwa katika ziara ya utalii wa ndani kama sehemu ya kuhamasisha watanzania kutembelea hifadhi ya Ruaha Iringa juzi (picha na Francis Godwin)






Hivyo makala WANYAMA HIFADHI YA RUAHA WAFA KWA KUKOSA MAJI

yaani makala yote WANYAMA HIFADHI YA RUAHA WAFA KWA KUKOSA MAJI Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala WANYAMA HIFADHI YA RUAHA WAFA KWA KUKOSA MAJI mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2019/02/wanyama-hifadhi-ya-ruaha-wafa-kwa.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "WANYAMA HIFADHI YA RUAHA WAFA KWA KUKOSA MAJI"

Post a Comment