title : SHILINGI BIL. 222 ZIMELIPWA KWA WAKULIMA WA KOROSHO-MAJALIWA
kiungo : SHILINGI BIL. 222 ZIMELIPWA KWA WAKULIMA WA KOROSHO-MAJALIWA
SHILINGI BIL. 222 ZIMELIPWA KWA WAKULIMA WA KOROSHO-MAJALIWA

Amesema wakulima walioanza kulipwa ni wale wenye kilo zisizozidi kilo 1,500 na wale wenye kilo zaidi ya 1,500 na kuendelea Serikali inaendelea na uhakiki kisha watalipwa.”Fedha zipo, hakuna mkulima ambaye atapoteza haki yake wote watalipwa. Tunaendelea na uhakiki kwa wale wenye korosho nyingi ili kubaini kama hawajanunua kangomba.”
Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili, Desemba 30, 2018) alipozungumza na wananchi wa kijiji cha Nandagala ‘A’ baada ya kufungua ofisi ya CCM kata ya Nandagala.Amesema baadhi ya watu wamekutwa na kilo zaidi ya 1,500 na wameshindwa kuonesha mashamba yao ya mikorosho, hali inayodhihirisha kwamba amenunua kupitia kangomba.
Waziri Mkuu amesema baadhi ya waliokutwa na korosho nyingi ni vijana wadogo ambao hawana hata uwezo kifedha hivyo Serikali itahakikisha inawakamata watu wanaowatuma.Amesema lengo la Serikali inayoongizwa na Rais Dkt. John Magufuli ni kuhakikisha wakulima wananufaika na kilimo chao, hivyo biashara ya kangomba lazima lidhibitiwe.Waziri Mkuu ambaye leo ameanza ziara yake kwa kikazi wilayani Ruangwa, Mkoani Lindi amesema zoezi la ulipaji kwa wakulima wa korosho linaendelea, wakulima wawe na subira.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>
Hivyo makala SHILINGI BIL. 222 ZIMELIPWA KWA WAKULIMA WA KOROSHO-MAJALIWA
yaani makala yote SHILINGI BIL. 222 ZIMELIPWA KWA WAKULIMA WA KOROSHO-MAJALIWA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala SHILINGI BIL. 222 ZIMELIPWA KWA WAKULIMA WA KOROSHO-MAJALIWA mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/12/shilingi-bil-222-zimelipwa-kwa-wakulima.html
0 Response to "SHILINGI BIL. 222 ZIMELIPWA KWA WAKULIMA WA KOROSHO-MAJALIWA"
Post a Comment