title : UCHAGUZI WA CHABATA KUFANYIKA OKTOBA 06 DODOMA
kiungo : UCHAGUZI WA CHABATA KUFANYIKA OKTOBA 06 DODOMA
UCHAGUZI WA CHABATA KUFANYIKA OKTOBA 06 DODOMA
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
BARAZA la Michezo la Taifa limetangaza uchaguzi mkuu wa Chama cha Baiskeli Tanzania (CHABATA) utakaotarajiwa kufanyika oktoba 06 mwaka huu katika Jiji la Dodoma.
Akizungumzia uchaguzi huo, Afisa habari wa BMT Najaha Bakari amesema kuwa fomu za uchaguzi zimeanza kutolewa katika ofisi za baraza hilo kuanzia leo hadi Oktoba Mosi mwaka huu.
Najaha amesema kuwa usaili utafanyika Oktoba 05 kuanzia saa 3 asubuhi kabla ya kufanyika kwa uchaguzi huo siku inayofuata katika nafasi za Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na wajumbe sita wa kuchaguliwa.
Najaha amesema sifa za wagombea hao ni lazima wawe na elimu ya kidato cha nne au zaifi, taaluma na uongozi katika mchezo wa baiskeli, awe raia wa Tanzania, awe na nidhamu pamoja na asiwe na historia ya kukutwa na hatia ya kufungwa zaidi ya miezi sita.
BMT imetoa wito kwa wenye nia ya dhati ya maendeleo ya mchezo huu, waone umuhimu wa kuchukua fomu na kugombea nafasi stahili ili kuendeleza chama cha michezo huu pamoja na kuiletea sifa nchi.
Mbali na hilo Najaha amewasihi viongozi wa vyama vya michezo kuona umuhimu wa kuwa na ofisi zao kwani kuanzia sasa hivi Baraza halitalifumbia macho suala hilo kwa kuona vyama havina ofisi wala hawajulikani wanapatikana wapi.
Hivyo makala UCHAGUZI WA CHABATA KUFANYIKA OKTOBA 06 DODOMA
yaani makala yote UCHAGUZI WA CHABATA KUFANYIKA OKTOBA 06 DODOMA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala UCHAGUZI WA CHABATA KUFANYIKA OKTOBA 06 DODOMA mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/08/uchaguzi-wa-chabata-kufanyika-oktoba-06.html
0 Response to "UCHAGUZI WA CHABATA KUFANYIKA OKTOBA 06 DODOMA"
Post a Comment