JUMAA AKABIDHI GARI YA WAGONJWA KWALA ILI KUPUNGUZA ADHA YA USAFIRI

JUMAA AKABIDHI GARI YA WAGONJWA KWALA ILI KUPUNGUZA ADHA YA USAFIRI - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa JUMAA AKABIDHI GARI YA WAGONJWA KWALA ILI KUPUNGUZA ADHA YA USAFIRI, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : JUMAA AKABIDHI GARI YA WAGONJWA KWALA ILI KUPUNGUZA ADHA YA USAFIRI
kiungo : JUMAA AKABIDHI GARI YA WAGONJWA KWALA ILI KUPUNGUZA ADHA YA USAFIRI

soma pia


JUMAA AKABIDHI GARI YA WAGONJWA KWALA ILI KUPUNGUZA ADHA YA USAFIRI

Na Mwamvua Mwinyi ,Kibaha Vijijini

MBUNGE wa jimbo la Kibaha Vijijini ,Hamoud Jumaa amekabidhi gari la wagonjwa (ambulance ),iliyogharimu mil.75 ,katika kituo cha afya cha Kwala .

Gari hiyo itaendelea kusaidia kupunguza adha ya usafiri kwa wagonjwa hasa mahututi na warufaa.Akikabidhi gari hilo ,kwa mganga mfawidhi wa kituo hicho ,diwani wa kata ya Kwala, mbele ya wananchi ,Jumaa alisema ataendelea kuwatumikia wananchi na kutatua kero zao .

"Serikali yetu inafanya makubwa katika kupunguza changamoto mbalimbali kwenye sekta ya afya na nyingine kama elimu ,miundombinu na nishati ya umeme""Kwa kutambua hayo ,July 2017 nilikabidhi magari mawili ya wagonjwa yaliyotokana na mfuko wangu na jingine moja ni msaada kutoka kwa Rais John Magufuli ikiwa ni kati ya magari ya wagonjwa 67 yaliyogawanywa katika maeneo mbalimbali nchini" alisema Jumaa.

Hata hivyo Jumaa ,alisema ameamua kujikita kutatua kero mbalimbali ili kwenda pamoja na kauli mbiu yake ya SISI KWANZA SERIKALI BAADAE .Mbunge huyo ,aliomba magari hayo yatunzwe na kutumike kwa matumizi lengwa.Nae mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kibaha,ambae pia ni diwani wa Kwala , Mansoor Kisebengo ,alisema hairuhusiwi wananchi kugharamia mafuta kwenye magari hayo .

Alielezea, halmashauri hiyo imekuwa inachangia gharama za mahitaji ya mafuta ili kuondoa bugudha kwa wananchi .Kwa upande wake mganga mfawidhi kituo cha afya Kwala ,dk.Mustapha Jaffar alimshukuru mbunge huyo kwa msaada alioutoa .Alisema hajafanya makosa kupeleka gari eneo la Kwala ,kwani litakuwa msaada mkubwa kwa wajawazito na wagonjwa wa rufaa.
Mbunge wa jimbo la Kibaha Vijijini ,Hamoud Jumaa akikabidhi funguo ya gari la wagonjwa ambalo limegharimu mil.75 ,kwa mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kibaha ,Mansoor Kisebengo ambae pia ni diwani wa kata ya Kwala.(picha na Mwamvua Mwinyi)
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kibaha ,Mansoor Kisebengo ambae pia ni diwani wa kata ya Kwala, akizungumza na wananchi wa Kwala ,kabla ya mbunge wa jimbo la Kibaha Vijijini ,Hamoud Jumaa kukabidhi gari la wagonjwa ambalo limegharimu mil.75 ,kwenye Kituo cha afya cha Kwala.(picha na Mwamvua Mwinyi)
Mbunge wa jimbo la Kibaha Vijijini ,Hamoud Jumaa akizungumza na wananchi wa Kwala kabla ya kukabidhi gari la wagonjwa ambalo limegharimu mil.75 ,katika kituo cha afya cha Kwala.


Hivyo makala JUMAA AKABIDHI GARI YA WAGONJWA KWALA ILI KUPUNGUZA ADHA YA USAFIRI

yaani makala yote JUMAA AKABIDHI GARI YA WAGONJWA KWALA ILI KUPUNGUZA ADHA YA USAFIRI Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala JUMAA AKABIDHI GARI YA WAGONJWA KWALA ILI KUPUNGUZA ADHA YA USAFIRI mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/08/jumaa-akabidhi-gari-ya-wagonjwa-kwala.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "JUMAA AKABIDHI GARI YA WAGONJWA KWALA ILI KUPUNGUZA ADHA YA USAFIRI"

Post a Comment