title : MRADI WA MAJI WA KIMBIJI NA MPERA UTASAIDIA UPATIKANAJI WA LITA MIL 260 KWA SIKU-PROF MBARAWA
kiungo : MRADI WA MAJI WA KIMBIJI NA MPERA UTASAIDIA UPATIKANAJI WA LITA MIL 260 KWA SIKU-PROF MBARAWA
MRADI WA MAJI WA KIMBIJI NA MPERA UTASAIDIA UPATIKANAJI WA LITA MIL 260 KWA SIKU-PROF MBARAWA
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof. Makame Mbarawa ametembelea mradi wa uchimbaji wa visima virefu vya Kimbijii na Mpera wenye thamani ya Bilioni 19.6 vitakavyosaidia kupatikana kwa lita za maji Milioni 260 kwa siku.
Mradi huo wa visima vya maji uliochini ya Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) una lengo la kuongeza wingi wa maji katika maeneo mbalimbali ya Jijini Dar es Salaam na kufikia lita Milioni 720 kwa siku kufikia mwaka 2032.
Prof Mbarawa akiwa ameongozana na Kaimu Mkurugenzi wa DAWASA Dkt Suphian Masasi ameweza kukagua visima hivyo na kuwataka wakandarasi wa mradi huo kuhakikisha unakamilika kwa wakati.
Akizungumza wakati wa kukagua visina hivyo, Prof Mbarawa amesema kuwa mradi huo utawasaidia wananchi wa Dar es Salaam kwa kuwa utasaidia upatikanaji wa maji safi na salama na yatakayotosheleza kwa matumizi yao.
" Mradi huu wa Kimbiji na Mpera utakaotoa Lita Milioni 260 kwa siku utasaidia sana wananchi wa Dar es Salaam, ukichukulia Mradi wa Ruvu Juu na Ruvu chini unatoa lita Milioni 502 kwa siku kwa ujumla wake utaleta chachu ksa wananchi kupata maji kwa uhakika,"amesema Prof Mbarawa.


WAZIRI Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa (katikati), akipata maelezo kutoka kwa Msimamizi wa miradi ya maji wa kampuni ya EGIS, Dk. Charles Kaaya, kuhusu kupima urefu wa kisima kirefu katika mradi wa maji wa visima virefu vya Kimbiji, wakati akikagua mradi huo Dar es Salaam. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa DAWASA, Dk. Suphian Masasi.
WAZIRI Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa akinywa maji katika moja ya Kisima ya miradi ya maji ya Kimbiji na Mpera wakati akikagua mradi huo Dar es Salaam. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa DAWASA, Dk. Suphian Masasi.
WAZIRI Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa akiwa pamoja Kaimu Mkurugenzi wa DAWASA, Dk. Suphian Masasikatika mradi wa maji wa visima virefu vya Kimbiji, wakati akikagua mradi huo Dar es Salaam utakaofanikisha upatikanaji wa lita Milioni 260 kwa siku.
Hivyo makala MRADI WA MAJI WA KIMBIJI NA MPERA UTASAIDIA UPATIKANAJI WA LITA MIL 260 KWA SIKU-PROF MBARAWA
yaani makala yote MRADI WA MAJI WA KIMBIJI NA MPERA UTASAIDIA UPATIKANAJI WA LITA MIL 260 KWA SIKU-PROF MBARAWA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala MRADI WA MAJI WA KIMBIJI NA MPERA UTASAIDIA UPATIKANAJI WA LITA MIL 260 KWA SIKU-PROF MBARAWA mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/07/mradi-wa-maji-wa-kimbiji-na-mpera.html
0 Response to "MRADI WA MAJI WA KIMBIJI NA MPERA UTASAIDIA UPATIKANAJI WA LITA MIL 260 KWA SIKU-PROF MBARAWA"
Post a Comment