WAZIRI LUKUVI KUONGOZA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA SHELTER AFRIQUE - KENYA

WAZIRI LUKUVI KUONGOZA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA SHELTER AFRIQUE - KENYA - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa WAZIRI LUKUVI KUONGOZA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA SHELTER AFRIQUE - KENYA, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : WAZIRI LUKUVI KUONGOZA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA SHELTER AFRIQUE - KENYA
kiungo : WAZIRI LUKUVI KUONGOZA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA SHELTER AFRIQUE - KENYA

soma pia


WAZIRI LUKUVI KUONGOZA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA SHELTER AFRIQUE - KENYA

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; William Lukuvi amekutana na viongozi wakuu wa Kampuni ya kuwezesha upatikanaji wa nyumba za bei nafuu – Shelter Afrique jijini Dar es Salaam.

Waziri Lukuvi alikutana na viongozi hao kwa kikao maalum ofisini kwake – Dar es Salaam. Viongozi hao ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo; Bwn. Femi Adowele na Katibu wake; Francesca Kakooza.Aidha, Suala mahususi lililowakutanisha viongozi hao lilikuwa ni kuhusu maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 37 wa Kampuni hiyo unaotegemewa kufanyika hivi karibuni nchini Kenya, ambapo Waziri Lukuvi ni Mwenyekiti wa Mkutano huo.

Kwa ujumla changamoto za nchi za kiafrika katika kuwapatia wananchi wa kawaida makazi nafuu zinafanana na kilio kikubwa katika nchi wanachama, ambazo ni kuwepo makazi holela hata baada ya nchi hizo kujikomboa kutoka ukoloni mkongwe. Shelter Afrique imedhamiria kuweka juhudi katika kuipa kipaumbele sekta ya Nyumba kwa kuwa ni sekta mtambuka katika kuharakisha ukuaji wa uchumi na maisha bora ya watu.

Mambo mbalimbali katika sekta ya Nyumba yanatarajiwa kuzungumziwa katika Mkutano huo wa 37, hususan katika jitihada za kupatikana kwa makazi bora na nafuu katika nchi wanachama, ambapo changamoto Kuu imekuwa ni Rasilimali fedha.Tanzania ni nchi mojawapo Mwanachama wa Shelter Afrique kati ya nchi 44 za barani Afrika .

Tanzania ilijiunga na Shelter Afrique mwaka 2003 na Mkutano wa 32 ambao ulifanyika N’djamena, Chad 2013, uliopitishwa na Azimio Namba GM/ 2013/005 la kuongeza Hisa kwa kila nchi mwanachama kwa lengo la kukuza mtaji wa Kampuni hiyo na kuiwezesha kuweka nguvu zaidi katika masuala ya uendelezaji nyumba barani Afrika. 

Mkutano wa mwaka huu wa 37, unategemewa kufanyika Nairobi, Julai 20, 2018.

Na kitengo cha Mawasiliano Serikalini – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi


Hivyo makala WAZIRI LUKUVI KUONGOZA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA SHELTER AFRIQUE - KENYA

yaani makala yote WAZIRI LUKUVI KUONGOZA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA SHELTER AFRIQUE - KENYA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala WAZIRI LUKUVI KUONGOZA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA SHELTER AFRIQUE - KENYA mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/06/waziri-lukuvi-kuongoza-mkutano-mkuu-wa_29.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "WAZIRI LUKUVI KUONGOZA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA SHELTER AFRIQUE - KENYA"

Post a Comment