MPINA ABARIKI NARCO KUVUNJA MKATABA WA MWEKEZAJI MZEMBE KATIKA RANCHI YA KAGOMA

MPINA ABARIKI NARCO KUVUNJA MKATABA WA MWEKEZAJI MZEMBE KATIKA RANCHI YA KAGOMA - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa MPINA ABARIKI NARCO KUVUNJA MKATABA WA MWEKEZAJI MZEMBE KATIKA RANCHI YA KAGOMA, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : MPINA ABARIKI NARCO KUVUNJA MKATABA WA MWEKEZAJI MZEMBE KATIKA RANCHI YA KAGOMA
kiungo : MPINA ABARIKI NARCO KUVUNJA MKATABA WA MWEKEZAJI MZEMBE KATIKA RANCHI YA KAGOMA

soma pia


MPINA ABARIKI NARCO KUVUNJA MKATABA WA MWEKEZAJI MZEMBE KATIKA RANCHI YA KAGOMA



Waziri
wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi  Luhaga
Mpina  ameridhia  maamuzi ya Kampuni ya Ranchi za NARCO kuvunja
mkataba baina ya mwekezaji Agri Vision Global Ltd na serikali  katika  Ranchi ya Kagoma  mkoani Kagera na kuamuru aondoka mara moja
baada ya mwekezaji huyo kushindwa kutekeleza mkataba huo katika kipindi cha
miaka mitano.

Waziri
Mpina ametoa maelekezo  hayo jana  alipotembelea Ranchi ya Kagoma kuangalia
shughuli mbalimbali  katika Ranchi hiyo
ambapo ametoa siku saba kwa mwekezaji huyo kuondoka katika eneo hilo na badala
yake Serikali kupitia NARCO kuendelea kusimamia shughuli za mifugo katika
Ranchi hiyo.

“Ninakuagiza  Mkuu wa Wilaya  kuanzia sasa 
hakikisha unaimarisha ulinzi katika ranchi hii katika kipindi cha
kukabidhi Ranchi baina ya Serikali na Mwekezaji 
ili kusitokee hujuma zozote” alisisitiza Mpina

Alitaja
baadhi ya mambo ambayo hayakutekelezwa na mwekezaji huyo kuwa ni pamoja na  kujenga 
machinjio ya nyama,  kujenga
kiwanda, kutoa gawio la shilingi bilioni tatu kila mwaka katika kipindi cha
miaka mitano, kutoa shilingi 2672 kwa hekta moja kama tozo la ardhi na
kushindwa kuendeleza miundombinu ya NARCO waliyoikuta wakati  wanaingia mikataba hiyo miaka mitano
iliyopita.

Waziri
Mpina  amemuagiza Meneja Mkuu wa NARCO,
Profesa  Philemoni Wambura  kuhakikisha kwamba ndani ya siku saba
anamleta Meneja katika Ranchi hiyo kwa ajili ya usimamizi wa shughuli za ranchi
hiyo na kuhakikisha kuwa inafanya kazi zake kisasa.

Aidha
Mpina ametoa siku saba  kwa   Uongozi wa NARCO kuhakikisha kuwa imefanya
tathmini  ya hasara zilizosababishwa na
mwekezaji huyo ili taratibu za kisheria zichukuliwe dhidi yake  ili aweze kuilipa Serikali ikiwa ni pamoja na
shilingi bilioni kumi na tano kama  gawio
la miaka mitano iliyokaa ambalo amesema halijawahi kulipwa hata shilingi moja.

“Sasa
tumeamua kuchukua hatua na tutaendelea kuchukua hatua kali dhidi ya wawekezaji
wasiowaaminifu wanaotaka kuihujumu serikali katika sekta hizi za mifugo na
Uvuvi” alihoji Mpina

Alionya
wawekezaji kuacha tabia ya kuidanganya serikali kwamba wanauwezo wa kuwekeza
katika vitalu  ili wapewe lakini wanabadili
matumizi baada ya kupewa. Aliongeza kwamba 
Serikali imegundua  baadhi ya
wawekezaji wanaopewa vitalu wanawakodisha wafugaji kutoka nchi jirani  na kujipatia faida wakati  Serikali haipati chochote.



Hivyo makala MPINA ABARIKI NARCO KUVUNJA MKATABA WA MWEKEZAJI MZEMBE KATIKA RANCHI YA KAGOMA

yaani makala yote MPINA ABARIKI NARCO KUVUNJA MKATABA WA MWEKEZAJI MZEMBE KATIKA RANCHI YA KAGOMA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala MPINA ABARIKI NARCO KUVUNJA MKATABA WA MWEKEZAJI MZEMBE KATIKA RANCHI YA KAGOMA mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/12/mpina-abariki-narco-kuvunja-mkataba-wa_6.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "MPINA ABARIKI NARCO KUVUNJA MKATABA WA MWEKEZAJI MZEMBE KATIKA RANCHI YA KAGOMA"

Post a Comment