title : MAFUNZO YA WISN NA POA YALIYOSHIRIKISHA MIKOA MINNE YAHITIMISHWA KWA MAFANIKIO.
kiungo : MAFUNZO YA WISN NA POA YALIYOSHIRIKISHA MIKOA MINNE YAHITIMISHWA KWA MAFANIKIO.
MAFUNZO YA WISN NA POA YALIYOSHIRIKISHA MIKOA MINNE YAHITIMISHWA KWA MAFANIKIO.
Na. Andrew Chimesela, Morogoro
Mafunzo ya kubaini mahitaji ya watumishi kwa kutumia mfumo unaojulikana kwa jina la kitaalamu Workload Indicators of Staffing Needs - WISN na Prioritaization and Optimization analysis – POA (WISN plus POA) yaliyoanza Juni 4 mwaka huu katika ukumbi wa ICE wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoinne – SUA Mkoani Morogoro yamehitimishwa Juni 8 kwa mafanikio makubwa.
Akiongea na washiriki wenzake wakati wa Kufunga mafunzo hayo Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Rasilimali Watu Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Sebastian Masanja amewapongeza wakufunzi wa mafunzo hayo kwa kujitahidi kuwapa kile walicholenga kutoa hadi wao kuelewa kwa ufanisi na kwa niaba ya wenzake ameahidi kwenda kuyafanyia kazi mafunzo hayo katika Halmashauri zao.
Bw. Masanja ambaye alikuwa mgeni rasimi katika kufunga mafunzo hayo amewataka washiriki wenzake kutambua kuwa hadi sasa watumishi wa Serikali hususan wa kada ya Afya bado hawatoshelezi kwenye vituo vya kutolea huduma, hivyo ni wajibu wao kutumia mafunzo waliyoyapata kuisaidia Serikali kuwapanga vizuri watumishi waliopo kulingana na uzinto wa kazi.
“Washiriki wenzangu, tumeshajifunza kuwa kituo cha Afya kilichopo Mjini hakiwezi kulingana majukumu yake na uzito wake wa kazi na kituo cha Afya cha kijijini, kwa sababu hata idadi ya wagonjwa inatofautiana, kwa hiyo tuisaidie Serikali kuondoa malalamiko kwa kuwapanga vizuri watumishi waliopo kulingana na uzito wa kazi zinazopatikana kwenye maeneo husika” alisema Bw. Masanja.
Baadhi ya timu ya viongoi wa mafunzo ya WISN PLUS POA wakiwa tayari kukabidhi vitabu vilivyoandaliwa kwa ajili ya kutekeleza kile walichojifunza washiriki wa mafunzo hayo. Kutoka kushoto ni Gracian Makota, Renatus Mashauri na Bw. Sebastian Masanja. Wengine ni wenyekiti wa washiriki wakati wa mafunzo na David Laput Mratibu wa PS 3 Mkoa wa Morogoro.
Bw. Sebastian Masanja ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala, Mkoa wa Kilimanjaro aliyefunga mafunzo hayo akimkabidhi vitabu Mmoja wa washiriki wa mafunzo ya WISN PLUS POA SUA Mkoani Morogoro. 
Mgeni Ramsi aliyefungua mafunzo ya WISN PLUS POA Dkt. Frank Jacob (katikati waliokaa) ambaye pia ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo hayo kutoka Mikoa ya Morogoro na Dodoma yaliyofanyika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine. Kwa habari kamili BOFYA HAPA
Hivyo makala MAFUNZO YA WISN NA POA YALIYOSHIRIKISHA MIKOA MINNE YAHITIMISHWA KWA MAFANIKIO.
yaani makala yote MAFUNZO YA WISN NA POA YALIYOSHIRIKISHA MIKOA MINNE YAHITIMISHWA KWA MAFANIKIO. Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala MAFUNZO YA WISN NA POA YALIYOSHIRIKISHA MIKOA MINNE YAHITIMISHWA KWA MAFANIKIO. mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/06/mafunzo-ya-wisn-na-poa-yaliyoshirikisha.html
0 Response to "MAFUNZO YA WISN NA POA YALIYOSHIRIKISHA MIKOA MINNE YAHITIMISHWA KWA MAFANIKIO."
Post a Comment