title : Ofisi ya Taifa ya Takwimu Yatoa Mafunzo ya Uandishi wa Habari za Takwimu
kiungo : Ofisi ya Taifa ya Takwimu Yatoa Mafunzo ya Uandishi wa Habari za Takwimu
Ofisi ya Taifa ya Takwimu Yatoa Mafunzo ya Uandishi wa Habari za Takwimu
………………
Na: Lilian Lundo – MAELEZO, Dodoma.
Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imetoa mafunzo ya uandishi wa habari za kitakwimu kwa wanachama wa chama cha waandishi wa habari Dodoma ili kuwaongezea uwezo wa uandishi mzuri wa habari za kitakwimu.
Mafunzo hayo ya siku mbili kuanzia tarehe 26 hadi 27 Mei, mwaka huu yanayofanyika katika ukumbi wa Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) Jijini Dodoma yamefunguliwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Zamaradi Kawawa kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara hiyo.
Akifungua mafunzo hayo Zamaradi Kawawa amesema kutokana na Wizara zote pamoja na baadhi ya Taasisi kuhamia Dodoma, Dodoma imekuwa ndio kitovu cha shughuli za Serikali kwa maana hiyo imekuwa chanzo kikuu cha habari zinazohusu Serikaki nchini hivyo basi majukumu ya vyombo vya habari vilivyopo mkoani Dodoma yameongezeka na yatazidi kuongezeka kadiri shughuli za Kiserikali zinavyoongezeka.
“Hapana shaka yeyote kuwa watumishi wote wa vyombo vya habari vilivyopo Dodoma wanahitaji mafunzo kama haya kwa ajili ya kuimarisha weledi wao katika kuripoti matukio mbalimbali yanayotokea mkoani humu,” amesema Zamaradi.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari MAELEZO Bi. Zamaradi Kawawa akifungua mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la Dodoma leo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi.
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari MAELEZO Bi. Zamaradi Kawawa akifungua mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la Dodoma leo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi.
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa akisisitiza kuhusu namna idadi ya watu inavyoongezeka au kupungua wakati wa mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la Dodoma leo.
Mtakwimu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Omary Mdoka akiwasilisha mada kuhusu ongezeko la watu wakati wa mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la Dodoma leo.
Mwanasheria wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Oscar Mangula akiwasilisha mada kuhusu Sheria ya takwimu ya mwaka 2015 wakati wa mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la Dodoma leo.
Mtakwimu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bi. Mariam Kitembe akisisitiza jambo wakati akiwasilisha mada kuhusu hali ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi hapa nchini kwa kuzingatia utafiti uliofanyika mwaka 2016/2017 wakati wa mafunzo ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la Dodoma leo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Said Ameir akitoa maelezo kuhusu mafunzo ya siku mbili ya uandishi wa habari za takwimu kwa waandishi wa habari wa Jiji la Dodoma leo.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Hivyo makala Ofisi ya Taifa ya Takwimu Yatoa Mafunzo ya Uandishi wa Habari za Takwimu
yaani makala yote Ofisi ya Taifa ya Takwimu Yatoa Mafunzo ya Uandishi wa Habari za Takwimu Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Ofisi ya Taifa ya Takwimu Yatoa Mafunzo ya Uandishi wa Habari za Takwimu mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/05/ofisi-ya-taifa-ya-takwimu-yatoa-mafunzo.html
0 Response to "Ofisi ya Taifa ya Takwimu Yatoa Mafunzo ya Uandishi wa Habari za Takwimu"
Post a Comment