title : ZITTO KABWE ATEMBELEA TUNDU LISU UBELIGIJI, WATETA MAKUBWA,.
kiungo : ZITTO KABWE ATEMBELEA TUNDU LISU UBELIGIJI, WATETA MAKUBWA,.
ZITTO KABWE ATEMBELEA TUNDU LISU UBELIGIJI, WATETA MAKUBWA,.


Mbunge Kigoma Mjini (ACT- Wazalendo), Zitto Kabwe amemtembelea Tundu Lissu nchini Ubelgiji anakoendelea na matibabu ya viungo na saikolojia tangu Januari 7, 2018.
Lissu ambaye ni mbunge wa Singida Mashariki anapata matibabu hayo baada ya kushambuliwa kwa risasi Septemba 7, 2017 akiwa nje ya makazi yake mjini Dodoma.
Awali mbunge huyo alipatiwa matibabu katika Hospitali ya Dodoma siku hiyohiyo kabla ya kuhamishiwa Hospitali ya Nairobi alikotobiwa hadi Januari 6, 2018 alipohamishiwa Ubelgiji.
Katika picha mbalimbali zilizotoka jana Februari 11, 2018 ziliwaonyesha wawili hao wakiwa kwenye mwonekano tofauti wa mazungumzo.
Leo Februari 12, 2018, Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Mawakili Tanzania (TLS) amesema, “Zitto amekuja kunijulia hali na kwa ajili ya kubadilishana mawazo kuhusu hali ya nchi yetu kisiasa, kiuchumi na kijamii.”
Hata hivyo, Zitto ambaye ni Kiongozi wa ACT- Wazalendo amesema hawezi kuzungumza zaidi kuhusu kile walichoteta na Lissu huku akiahidi baadaye kutoa taarifa
Hivyo makala ZITTO KABWE ATEMBELEA TUNDU LISU UBELIGIJI, WATETA MAKUBWA,.
yaani makala yote ZITTO KABWE ATEMBELEA TUNDU LISU UBELIGIJI, WATETA MAKUBWA,. Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala ZITTO KABWE ATEMBELEA TUNDU LISU UBELIGIJI, WATETA MAKUBWA,. mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/02/zitto-kabwe-atembelea-tundu-lisu.html
0 Response to "ZITTO KABWE ATEMBELEA TUNDU LISU UBELIGIJI, WATETA MAKUBWA,."
Post a Comment