DED UKEREWE APEWA SIKU TATU KUELEZA MATUMIZI YA SH. MIL. 350 ZA MIRADI YA MAENDELEO

DED UKEREWE APEWA SIKU TATU KUELEZA MATUMIZI YA SH. MIL. 350 ZA MIRADI YA MAENDELEO - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa DED UKEREWE APEWA SIKU TATU KUELEZA MATUMIZI YA SH. MIL. 350 ZA MIRADI YA MAENDELEO, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : DED UKEREWE APEWA SIKU TATU KUELEZA MATUMIZI YA SH. MIL. 350 ZA MIRADI YA MAENDELEO
kiungo : DED UKEREWE APEWA SIKU TATU KUELEZA MATUMIZI YA SH. MIL. 350 ZA MIRADI YA MAENDELEO

soma pia


DED UKEREWE APEWA SIKU TATU KUELEZA MATUMIZI YA SH. MIL. 350 ZA MIRADI YA MAENDELEO

 Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ukerewe, Frank Bahati akijibu maswali aliyoulizwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika mkutano kati ya Waziri Mkuu na watumishi wa Halmashauri hiyo
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua  madawati  ya madarasa ya Kidato cha Tano na Sita katika Shule ya Sekondari ya Pius  Msekwa wilayani Ukerewe Februari 18, 2018. Wanne kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikata utepe kuzindua mabweni mawili ya Kidato cha Tano na Sita katika Shule ya Sekondari ya Pius Msekwa wilayani Ukerewe Februari 18, 2018. Wasita kulia ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina na watatu kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella.
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua mradi wa maji katika kijiji cha Bwasa wilayani Ukerewe
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akijaza  maji katika ndoo ya Janet Magayi (kushoto) wakati alipozindua  mradi wa maji katika kijiji cha Bwasa wilayani Ukerewe, akiwa katika ziara ya mkoa wa Mwanza.
Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa siku tatu kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Ukerewe Bw. Frank Bahati aeleze amepeleka wapi zaidi ya sh milioni 350 zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya miradi mbalimbali. 
Ametoa agizo hilo Jumapili Februari 18, 2018 wakati akizungumza na madiwani na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe akiwa katika siku ya nne ya ziara yake ya kikazi mkoani Mwanza. 
Waziri Mkuu amesema Serikali haiwezi kuvumia kuona fedha inazopeleka katika halmashauri hiyo kwa ajili ya kugharamia miradi na kulipa madai ya watumishi zinatumika kinyume na maelekezo. 
Amesema miongoni mwa fedha hizo ni sh. milioni 451.47 za miradi ya miradi ya maendeleo (CDG), ambapo zilizotumika ni sh. milioni 221.9 tu.” Namtaka Mkurugenzi na Muweka hazina wa Halmashauri hii Bw. Peter Molel tarehe 21 waje Mwanza wanieleze walikopeleka fedha hizo.” 
Waziri Mkuu amesema fedha zingine ni sh. milioni 50 za ziizotolewa na Serikali kwa ajili ya kulipa madai mbalimbali ya watumishi kama likizo ambapo zililipwa sh. milioni 13 na zingine hazijulikani zilipo. 
Pia Serikali ilitoa sh. milioni 65 za kugharamia mradi wa umwagiliaji wa Bugorola ambazo nazo hazijulikani zilipo pamoja na sh. milioni 84 zilizotolewa kwa ajili ya kulipa motisha kwa walimu ambapo zilizolipwa ni sh. milioni 60 tu. 
“Kama mlidhani Ukerewe ni sehemu ya kutafunia fedha za umma mmekosea kwa sababu Serikali haiwezi kuvumia haya, Mkurugenzi umeaminika na kupewa dhamana ya kusimamia rasilimali za umma lakini unafanya tofauti.”
Waziri Mkuu amesisitiza kwamba lazima viongozi hao wahakikishe fedha zinazopelekwa na Serikali katika Halmashauri zao zikiwemo za utekelezaji wa miradi ya afya, elimu, uvuvi zinatumika kama ilivyoelekezwa na si vinginevyo. 
Pia Waziri Mkuu amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza asimamie utendaji wa viongozi na watumishi katika  wilaya zote za mkoa huo na kisha kutoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa, Bw. John Mongella. 
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka watumishi wa Halmashauri hiyo wasikubali kugawanywa kwa sababu ya maslahi ya watu ambayo hayana tija kwao na hata kwa wananchi wa wilaya hiyo.  
Waziri Mkuu ameyasema hayo baada ya kubaini kuwepo kwa mgogoro kati ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bw. Bahari pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Bw. George Nyamaha ambao wamekuwa wakiwagawa watumishi. 
Amewataka viongozi hao kurekebisha tofauti zao kwa sababu mgogoro wao umesababisha watumishi kugawanyika, hivyo kuwaumiza wananchi wa wilaya ya Ukerewe kwa kushindwa kuwahudumia vizuri jambo ambalo halikubaliki.


Hivyo makala DED UKEREWE APEWA SIKU TATU KUELEZA MATUMIZI YA SH. MIL. 350 ZA MIRADI YA MAENDELEO

yaani makala yote DED UKEREWE APEWA SIKU TATU KUELEZA MATUMIZI YA SH. MIL. 350 ZA MIRADI YA MAENDELEO Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala DED UKEREWE APEWA SIKU TATU KUELEZA MATUMIZI YA SH. MIL. 350 ZA MIRADI YA MAENDELEO mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/02/ded-ukerewe-apewa-siku-tatu-kueleza.html

Subscribe to receive free email updates:

0 Response to "DED UKEREWE APEWA SIKU TATU KUELEZA MATUMIZI YA SH. MIL. 350 ZA MIRADI YA MAENDELEO"

Post a Comment