title : MCB YAZINDUA BIDHAA ‘TUKUTANE JANUARI’
kiungo : MCB YAZINDUA BIDHAA ‘TUKUTANE JANUARI’
MCB YAZINDUA BIDHAA ‘TUKUTANE JANUARI’
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Benki ya ya Mwalim Commercial (MCB) imezindua bidhaa ya Tukutane Januari kwa ajili ya mkakati wa kuboresha maisha ya watanzaia.
Akizungumza na waandishi habari katika uzinduzi wa bidhaa hiyo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa MCB , Ronald Manongi amesema kuanzishwa kwa bidhaa hiyo ni kwa ajili kuwasaidia watanzania wasipate shida kila inapofika Januari.
Manongi amesema kuwa mteja ataweza kujiwekea akiba kidogo kidogo wakati wowote katika kipindi chote cha hadi Januari.Amesema akaunti hiyo ina riba ya kuvutia ambayo mteja atalipwa riba kila robo ya mwaka pamoja na kumfanya mteja kukopa wa hadi asilimia 30 ya amana yake katika kipindi cha mwaka husika.
Aidha amesema faida ya akaunti hiyo itamuondolea usumbufu wa kutatua mahitaji muhimu ya kipesa katika kipindi cha mwanzo wa mwaka husika ikiwa ni pamoja na ada za shule , vyuo , vifaa vya shule , kodi za nyumba .
Manongi amesema amewasaa watanzania kujenga utamaduni wa kuweka akiba mara kwa mara kwani husaidia kutatua matatizo mengi yanayowakabili.
Mkurugenzi Mkuu wa Mkuu wa Mwalimu Commercial Benki (PLC), Ronald Manongi (katika)akizungumza na waandishi habari kuhusiana na uzinduzi wa bidhaa mpya ya Tukutane Januari leo jijini Dar es Salaam.kushoto ni Meneja wa Tawi la Samora, Leticia Ndogole na kulia ni Mkurugenzi wa Ukuzaji wa Biashara na Masoko Valence Luteganya
Hivyo makala MCB YAZINDUA BIDHAA ‘TUKUTANE JANUARI’
yaani makala yote MCB YAZINDUA BIDHAA ‘TUKUTANE JANUARI’ Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala MCB YAZINDUA BIDHAA ‘TUKUTANE JANUARI’ mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/01/mcb-yazindua-bidhaa-tukutane-januari.html
0 Response to "MCB YAZINDUA BIDHAA ‘TUKUTANE JANUARI’"
Post a Comment