RC MAKONDA AKAGUA UJENZI WA JENGO LA HUDUMA ZA DHARULA HOSPITAL YA TEMEKE.

RC MAKONDA AKAGUA UJENZI WA JENGO LA HUDUMA ZA DHARULA HOSPITAL YA TEMEKE. - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa RC MAKONDA AKAGUA UJENZI WA JENGO LA HUDUMA ZA DHARULA HOSPITAL YA TEMEKE., tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : RC MAKONDA AKAGUA UJENZI WA JENGO LA HUDUMA ZA DHARULA HOSPITAL YA TEMEKE.
kiungo : RC MAKONDA AKAGUA UJENZI WA JENGO LA HUDUMA ZA DHARULA HOSPITAL YA TEMEKE.

soma pia


RC MAKONDA AKAGUA UJENZI WA JENGO LA HUDUMA ZA DHARULA HOSPITAL YA TEMEKE.



Mwambawahabari
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda leo amekagua ujenzi wa Jengo la Huduma Dharura  ya kwenye Hospital ya Rufaa Temeke ambayo Ujenzi wake unafadhiliwa na  Ubalozi wa Japan Nchini Tanzania

Ujenzi wa Jengo hilo unagharimu kiasi cha  Shillingi Million 800  ambazo ni matunda ya  jitiada binafsi za RC Makonda baada ya kumtafuta Balozi wa Japan Nchini Tanzania na kumueleza changamoto ya ukosefu wa kitengo cha Huduma za haraka kwenye Hospital za Mkoa ambapo  baada ya mazungumzo Balozi alipokea kwa mikono miwili ombi la RC Makonda.

RC Makonda, amesema  kukamilika kwa jengo hilo itasaidia kupunguza Vifo vitokanavyo na Wagonjwa wanaohitaji huduma ya haraka kuikosa huduma hiyo kwa uharaka.

Amesema jengo hilo ni mahususi kwajili ya wagonjwa wote wanaohitaji huduma ya haraka hususani Majeruhi wa Ajali, Wanaougua Malaria kali ya gafla, Maumivu ya Tumbo, wanaobanwa na Kifu, Wajawazito, Homa kali, ajali ya Moto na Magonjwa yote yanayohitaji huduma ya haraka.

Amebainisha kuwa  wagonjwa wanaohitaji huduma ya haraka  wanaofikishwa Hospitalini hapo wamekuwa wakipelekwa Hospital ya Muhimbili ambako ni mbali kutoka Temeke hivyo kusababisha wengi wao kupoteza maisha Barabarani.

Aidha  Makonda, amesema baada ya kumalizika kwa jengo hilo  ujenzi wa majengo ya huduma ya haraka utahamia kwenye Hospital ya Amana na Mwananyamala ilikuipungizia mzigo Muhimbili

Kwa upande wake  Mganga Mfawidhi wa Hospital ya Temeke Dr. Aman Malima amesema kwa siku wanapokea  wagonjwa kati ya 1,800 -2,000 ambapo kati ya hao 200 ni wagonjwa wanaohitaji huduma ya dharura  hivyo amesema uwepo wa huduma hiyo itasaidia kuokoa maisha.

Amempongeza RC Makonda kwa juhudi zake binafsi za kutafuta wadau waliofanikisha ujenzi wa Jengo hilo.

Nae Mkandarasi wa ujenzi huo Bwana Abdulkadir Msangi  amesema ujenzi umefikia  85%  ambapo hadi kufikia mwishoni mwa  Mwezi November ujenzi utakuwa umekamilika na jengo kukabidhiwa.


Hivyo makala RC MAKONDA AKAGUA UJENZI WA JENGO LA HUDUMA ZA DHARULA HOSPITAL YA TEMEKE.

yaani makala yote RC MAKONDA AKAGUA UJENZI WA JENGO LA HUDUMA ZA DHARULA HOSPITAL YA TEMEKE. Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala RC MAKONDA AKAGUA UJENZI WA JENGO LA HUDUMA ZA DHARULA HOSPITAL YA TEMEKE. mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/10/rc-makonda-akagua-ujenzi-wa-jengo-la.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "RC MAKONDA AKAGUA UJENZI WA JENGO LA HUDUMA ZA DHARULA HOSPITAL YA TEMEKE."

Post a Comment