Matukio : Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania kuutangaza Utalii wa Tanzania katika ziara ya Thailand

Matukio : Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania kuutangaza Utalii wa Tanzania katika ziara ya Thailand - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Matukio : Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania kuutangaza Utalii wa Tanzania katika ziara ya Thailand, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Matukio : Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania kuutangaza Utalii wa Tanzania katika ziara ya Thailand
kiungo : Matukio : Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania kuutangaza Utalii wa Tanzania katika ziara ya Thailand

soma pia


Matukio : Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania kuutangaza Utalii wa Tanzania katika ziara ya Thailand





Na Richard Mwaikenda
Akizungumza mjini Dar es Salaam wakati wa kikao cha maandalizi na baadhi ya Wana Mkikita watakaokwenda Thailand, Mtaribu wa ziara hiyo, Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kampuni ya Resorce Afrika Limited, Idrissa Songoro amesema kuwa maandalizi ya ziara hiyo kwa upande wa Thailand kwa asilimia kubwa yako tayari.
Amesema kuwa ziara hiyo ya wiki moja Wanamkikita watanufaika kwa mambo mengi, ambapo licha ya kutangaza vivutia mbalimbali vya utalii pia wataonesha utamaduni wa mapishi ya kila aina ya vyakula vya asili vya Kitanzania.
Amesema Wanamkikita ambao miongoni mwao ni Wakulima, Wafanyabiashara na Wajasiriamali watapata wasaa wa kubadilishana mawazo na wenzao wa Thailand kwa lengo la kukuza ushirikiano katika masuala ya kibiashara,kilimo cha kisasa na ufugaji wa kisasa.
Songoro amewaasa Wanamkikita kufanya maandalizi ya uhakika ili wakienda Thailand wanufaike na ziara hiyo na kuwa na mrejesho mzuri watakaporejea nyumbani.



"Kitabia Wathailand wanafanana na Watanzania, kwani ni wakalimu, wapole, waungwana lakini pia ni wachapakazi na wako makini sana katika kila jambo wanalolifanya,"amesema Songoro.




Amesema kuwa Ujumbe huo utapata pia fursa ya kutembelea eneo la viwanda, mashamba ya wakulima pamoja na eneo la utafiti wa kilimo la Chiang Mai na Mji Mkuu wa Bangkok.




"Wathailand wana elimu mkubwa katika nyanja ya uhifadhi wa vyakula na kuviongezea thamani pamoja na kutangaza logo za kibiashara,. Pia wana mbegu za mazao mbalimbali zinazotoa mazao mengi kwa hekali, kwa mfano unaweza kuzalisha kabeji tani 25 kwa heka moja,"amesema Songoro.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Mkikita, Dk. Kisui S. Kisui aliwaasa Wanamkikita kuichangamkia ziara hiyo kwani watakaokwenda watanufaika kwa kupata fursa mbalimbali za maendeleo ikiwemo masuala ya kilimo cha kisasa na biashara.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao huo, Adam Ngamange alielezea jinsi Mkikita ilivyopanga kuwaandaa wanajachama watakao kwenda huko kwa kuwapiga msasa kwa kutumia vikao na semina mbalimbali ili wawe na uelewa kwa kujua mambo mbalimbali watakayokwenda kufanya katika ziara hiyo muhimu.
Aliimpongeza Songoro kwa jitihada zake kwa kujitolea kwa moyo mkunjufu kuratibu ziara hiyo itakayokuwa na makubwa kwa Mkikita, Wanachama na Tanzania kwa ujumla.

Mtaribu wa ziara hiyo, Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kampuni ya Resorce Afrika Limited, Idrissa Songoro akizungumza kuhusu maandalizi ya ziara ya mafunzo ya Wanachama wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (MKIKITA),nchi Thailand inayotarajia kuanza katilati ya mwezi ujao Novemba mwaka huu. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao huo, Adam Ngamange na Mwenyeikiti wa Bodi ya Mkikita, Dk. Kisui . Kisui.UJUMBE wa Wanachama wa Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (MKIKITA) unaokwenda ziara ya mafunzo nchini Thailand, umejiandaa pia kwenda kuutangaza utalii wa Tanzania.

Songoro na viongozi wa Mkikita wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wanamkikita wanaotarajia kwenda Thailand kwa ziara ya wiki moja.

Dk. Kisui akielezea jinsi Mkikita ulivyojipanga kwa ziara hiyo, itakayowanufaisha wanachama kwa kukutana ana kwa anakwa mazungmzo na wafanyabiashara na wakulima wa Thailand pamoja na kuingia nao mikataba mbalimbali.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mkikita, Ngamange akifafanua jambo kwa wajumbe

Ngamange akiwa na baadhi ya Wajumbe wa Bodi ya Mkikita wakati wa kikao hicho

Baadhi ya wajumbe wakiwa katika kikao wakimsikiliza Songoro







Songoro akifafanua jambo katika kikao hicho

Ngamange akitoa shukrani kwa Songoro kwa uratibu wa ziara hiyo pamoja na kukubali kushiriki kwenye kikao hicho




Elizabeth Ndangoba Mkurugenzi wa Fedha na Utawalawa Mkikita

Catherine Edward Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mkikita

Adam Ngamange

Dk. Kisui akisisitiza jambo alipokuwa akifunga kikao hicho

Songoro akijadiliana mambo na wajumbe wa Mkikita

Mjasiriamali Mwambapa akiwa na Ngamange

Songoro akihojiwa na African Swahili Televisheni

Ngamange, Rose na Dk Kisui

Songoro akiwa na Mwambapa pamoja na Ngamange.
PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA
-KAMANDA WA MATUKIO BLOG


Hivyo makala Matukio : Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania kuutangaza Utalii wa Tanzania katika ziara ya Thailand

yaani makala yote Matukio : Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania kuutangaza Utalii wa Tanzania katika ziara ya Thailand Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Matukio : Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania kuutangaza Utalii wa Tanzania katika ziara ya Thailand mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/10/matukio-mtandao-wa-kijani-kibichi.html

Subscribe to receive free email updates:

0 Response to "Matukio : Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania kuutangaza Utalii wa Tanzania katika ziara ya Thailand"

Post a Comment