title : Tanzania Yawa Mwenyeji wa Mkutano wa 37 wa Madini Afrika
kiungo : Tanzania Yawa Mwenyeji wa Mkutano wa 37 wa Madini Afrika
Tanzania Yawa Mwenyeji wa Mkutano wa 37 wa Madini Afrika
Tanzania imekuwa Mwenyeji wa Mkutano wa 37 wa Masuala ya Kisera ya Kituo cha Afrika cha Sayansi ya Jiolojia na Madini (African Minerals and Geosciences Center (AMGC) ambao unafanyika jijin Dar es Salaam.
Awali, mkutano huo ulianza kwa kuwakutanisha Wakurugenzi wa Bodi ya kituo hicho na kufuatiwa na mkutano wa tarehe 13 Agosti, 2017, uliowashirikisha Makatibu Wakuu kutoka nchi Wanachama wa kituo husika.
Akizungumza na Vyombo vya Habari wakati wa Mkutano wa Makatibu Wakuu, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Prof. James Mdoe alisema lengo la kukutana ni kufanya tathmini na kuendeleza yale yaliyopangwa kutekelezwa na nchi wanachama ikiwemo kupanga mipango ya mwaka ujao na bajeti ya utekelezaji wa mipango hiyo.
Profesa Mdoe alisema kuwa yapo mambo ambayo waliyokubaliana katika mkutano wa 36 yakiwemo ujenzi ya Maabara ya kisasa kwa ajili ya nchi za Maziwa Makuu ambayo itasaidia katika shughuli za madini ikiwemo za uchunguzi wa madini, kukiwezesha kituo hicho kufanya shughuli zake vizuri na kusaidia nchi wanachama katika sekta husika.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe (katikati mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja ya Mkutano wa MakatibU Wakuu kutoka Nchi Wanachama wa Kituo cha Afrika cha Sayansi ya Jiolojia na Madini (AMGC). Wengine katika picha ni wawakilishi kutoka Nchi wanachama pamoja Makamishna na Wakuu wa Vituo vya Madini.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe (katikati) baada ya kufugua kikao cha Makatibu Wakuu kutoka Nchi Wanachama wakiwa katika Kituo cha Afrika Sayansi ya Jiolojia na Madini (AMGC). Wengine ni Kamishna wa Madini, Mhandisi Benjamin Mchwampaka (kushoto) na Assa Mwakilembe (kulia).
Baadhi ya wawakilishi wa Bodi ya Kituo cha Afrika cha Sayansi ya Jiolojia na Madini (AMGC), wa kwanza kutoka kulia ni Mwenyekiti wa UNECA, Dkt. Koja Busia, Mwenyekiti wa Bodi, Masresha Gebreselassie, Mwenyekiti wa AUC, Frank Mugyenyi na Mkurugenzi Mkuu wa AMGC, Ibrahim Shaddad.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa James Mdoe (anayeongea). Wengine ni washiriki katika kikao hicho.
Hivyo makala Tanzania Yawa Mwenyeji wa Mkutano wa 37 wa Madini Afrika
yaani makala yote Tanzania Yawa Mwenyeji wa Mkutano wa 37 wa Madini Afrika Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Tanzania Yawa Mwenyeji wa Mkutano wa 37 wa Madini Afrika mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/09/tanzania-yawa-mwenyeji-wa-mkutano-wa-37.html
0 Response to "Tanzania Yawa Mwenyeji wa Mkutano wa 37 wa Madini Afrika"
Post a Comment