title : DEREVA WA MBUNGE WA CHADEMA AKATWA MAPANGA HUKO TARIME
kiungo : DEREVA WA MBUNGE WA CHADEMA AKATWA MAPANGA HUKO TARIME
DEREVA WA MBUNGE WA CHADEMA AKATWA MAPANGA HUKO TARIME
Dereva wa Mbunge John Heche (CHADEMA) amevamiwa usiku wa kuamkia leo Ijumaa Septemba 15,2017 na watu wasiojulikana na kukatwa mapanga Mjini Tarime ambapo inaelezwa kuwa hali yake siyo nzuri.
Tukio hilo limetokea jana majira ya saa mbili usiku ambapo dereva huyo anadaiwa kukatwa mapanga kichwani.
Mbunge John Heche amethibitisha kutokea kwa tukio hilo kutokana na taarifa alizopata kupitia Katibu wake, Mrimi Zablon ambaye amekiri Dereva huyo anayefahamika kwa jina la Suez Daniel Maradufu ni kweli amepata shambulio hilo na sasa yupo hospitali akipatiwa matibabu.
Kwa upande wa Kamanda wa Polisi Tarime Rorya, SACP Henry Mwaibambe alipotafutwa kwa njia ya simu na Mwandishi wetu amesema yupo kwenye kikao na akimaliza atatoa ripoti kamili.
Dereva huyo amelazwa katika hospitali ya Bomani Tarime mkoani Mara.
Hivyo makala DEREVA WA MBUNGE WA CHADEMA AKATWA MAPANGA HUKO TARIME
yaani makala yote DEREVA WA MBUNGE WA CHADEMA AKATWA MAPANGA HUKO TARIME Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala DEREVA WA MBUNGE WA CHADEMA AKATWA MAPANGA HUKO TARIME mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/09/dereva-wa-mbunge-wa-chadema-akatwa.html
0 Response to "DEREVA WA MBUNGE WA CHADEMA AKATWA MAPANGA HUKO TARIME"
Post a Comment