TAMASHA LA BODABODA KUFANYIKA MEI 13

TAMASHA LA BODABODA KUFANYIKA MEI 13 - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa TAMASHA LA BODABODA KUFANYIKA MEI 13, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : TAMASHA LA BODABODA KUFANYIKA MEI 13
kiungo : TAMASHA LA BODABODA KUFANYIKA MEI 13

soma pia


TAMASHA LA BODABODA KUFANYIKA MEI 13


Mwambawahabari
MAKAMPUNI ya JP Decaux pamoja na International Republican Institute (IRI) yameandaa Tamasha la waendesha pikipiki linalotarajia kufanyika Mei 13 mwaka huu katika viwanja vya Tanganyika Parkers Jijini Dar es Salaam.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya JP Decaux, Shaban Makugaya wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya tamasha hilo.

“Lengo la tamasha hili ni kuweka uamsho, msisitizo na kuendelea kutoa elimu ya usalama barabarani kwa madereva wa pikipiki na abiria kwa dhumuni la kuzingatia sheria za usalama kwa matumizi ya barabara pamoja na kudumisha umoja, ushirikiano na mshikamano katika jamii”. Alisema Makugaya.

Aidha, Makugaya amesema kuwa, tamasha hilo ni la kwanza kufanyika nchini na Kampuni hiyo imejipanga kulifanya kila mwaka nchi nzima ambapo jina la maonesho litabadilika kulingana na mji au mkoa ambao tamasha litafanyika.

Aliongeza kuwa usafiri wa pikipiki umekua njia rahisi za kumuwezesha msafiri kufika haraka hivyo mashirika hayo yameamua kuwakutanisha madereva hao na kuwapa elimu ya usalama barabarani ili waweze kuepuka ajali za barabarani zinazosababisha vifo vya watanzania wengi.

Akifafanua zaidi, Mkurugenzi huyo amesema kuwa waendesha bodaboda watakaoshiriki katika tamasha hilo ni lazima wawe na leseni na watoke katika vikundi vyao vilivyosajiliwa na kutambulika kisheria.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya JP Decaux, Elia Moshi amesema tamasha hilo litahusisha michezo mbalimbali ikiwemo ya soka kati ya timu ya trafiki na waendesha pikipiki, burudani ya mziki wa kizazi kipya, taarabu na singeli pia zitakuwepo ili kuboresha tamasha hilo.

“Tamasha hili litafayika mkoani Dar es Saaam pekee na linatarajia ushiriki wa watu kati ya 5000 na kuendelea ambapo mshindi wa kwanza atajipatia pikipiki pamoja na fedha taslimu na kutakua na zawadi zingine kwa ajili ya washindi wengine pamoja na washiriki,” alisema Moshi.

Bodaboda Superstar ni onesho linalojumuisha burudani na elimu ambalo limelenga kuwaleta pamoja waendesha pikipiki na wananchi ambapo Kauli mbiu ya tamasha hilo ni ‘Sote ni Ndugu’. 


Hivyo makala TAMASHA LA BODABODA KUFANYIKA MEI 13

yaani makala yote TAMASHA LA BODABODA KUFANYIKA MEI 13 Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala TAMASHA LA BODABODA KUFANYIKA MEI 13 mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2017/04/tamasha-la-bodaboda-kufanyika-mei-13_27.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "TAMASHA LA BODABODA KUFANYIKA MEI 13"

Post a Comment