TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA 26 KUHUSU MIFUMO YA USAFIRISHAJI UMEME

TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA 26 KUHUSU MIFUMO YA USAFIRISHAJI UMEME - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA 26 KUHUSU MIFUMO YA USAFIRISHAJI UMEME, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA 26 KUHUSU MIFUMO YA USAFIRISHAJI UMEME
kiungo : TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA 26 KUHUSU MIFUMO YA USAFIRISHAJI UMEME

soma pia


TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA 26 KUHUSU MIFUMO YA USAFIRISHAJI UMEME

Na Veronica Simba – Entebbe
Kamishan wa Umeme na Nishati Mbadala, Mhandisi Innocent Luoga, kutoka Wizara ya Nishati, ameongoza timu ya wataalamu wa nishati kutoka Tanzania, kushiriki katika mkutano wa 26 wa Kamati Tendaji unaojadili mifumo ya kusafirisha umeme, iliyounganishwa katika nchi zilizopo Mashariki mwa Afrika (Eastern Africa Power Pool – EAPP)

Mkutano huo unaofanyika leo, Februari 20, katika mji wa Entebbe nchini Uganda, ni wa ngazi ya wataalamu kutoka nchi wanachama, ukiwa ni utangulizi wa mkutano wa 14 wa Baraza la Mawaziri wa sekta husika unaotarajiwa kufanyika kesho, Februari 21, 2019.

Miongoni mwa masuala yanayojadiliwa, ni pamoja na maboresho ya mkataba wa ushirikiano kwa nchi wanachama wa EAPP. Aidha, mkutano unajadili masuala ya biashara ya kuuziana na kusafirisha umeme kupitia mifumo ya EAPP na SAPP (Southern Africa Power Pool). Nchi wanachama wa EAPP ni Tanzania, Uganda, Kenya, Ethiopia, Libya, Sudan, Misri, Rwanda, DRC na Djibouti.

Mbali na Kamishna Luoga, wataalamu wengine wanaoshiriki mkutano huo kutoka Tanzania ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Dkt. Tito Mwinuka, Mhandisi Christopher Bitesigirwe kutoka Wizara ya Nishati, Mhandisi Meksesius Kalinga kutoka TANESCO pamoja na Mhandisi Pius Gaspar kutoka TANESCO.

Katika mkutano wa 14 wa Baraza la Mawaziri hapo kesho, Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu atamwakilisha Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani.
 Timu ya wataalamu wa nishati kutoka Tanzania, inayoshiriki katika mkutano unaojadili kuhusu mifumo ya kusafirisha umeme iliyounganishwa katika nchi za Mashariki mwa Afrika (Eastern Africa Power Pool – EAPP), mjini Entebbe, Uganda. Kamishna wa Umeme na Nishati Mbadala, Mhandisi Innocent Luoga (katikati), Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt. Tito Mwinuka (wa pili – kulia), Mhandisi Christopher Bitesigirwe kutoka Wizara ya Nishati (kulia), Mhandisi Meksesius Kalinga kutoka TANESCO (kushoto) pamoja na Mhandisi Pius Gaspar kutoka TANESCO (wa pili - kushoto).
 Wataalamu wa nishati kutoka nchi wanachama wa Eastern Africa Power Pool (EAPP), wakiwa katika picha ya pamoja, kabla ya kuanza mkutano wao uliojadili masuala mbalimbali kuhusu mifumo ya kusafirisha umeme iliyounganishwa katika nchi husika. Mkutano huo umefanyika Februari 20, 2019 mjini Entebbe, Uganda.
 Kamishna wa Umeme na Nishati Mbadala, Mhandisi Innocent Luoga, akiwa katika mkutano wa 26 wa Kamati Tendaji unaojadili mifumo ya kusafirisha umeme, iliyounganishwa katika nchi zilizopo Mashariki mwa Afrika (Eastern Africa Power Pool – EAPP)
 Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt. Tito Mwinuka (wa kwanza – kulia), akiwa katika mkutano wa 26 wa Kamati Tendaji unaojadili mifumo ya kusafirisha umeme, iliyounganishwa katika nchi zilizopo Mashariki mwa Afrika (Eastern Africa Power Pool – EAPP).
Mhandisi Christopher Bitesigirwe kutoka Wizara ya Nishati (kushoto) na Mhandisi Meksesius Kalinga kutoka TANESCO (kulia), wakiwa katika mkutano wa 26 wa Kamati Tendaji unaojadili mifumo ya kusafirisha umeme, iliyounganishwa katika nchi zilizopo Mashariki mwa Afrika (Eastern Africa Power Pool – EAPP).



Hivyo makala TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA 26 KUHUSU MIFUMO YA USAFIRISHAJI UMEME

yaani makala yote TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA 26 KUHUSU MIFUMO YA USAFIRISHAJI UMEME Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA 26 KUHUSU MIFUMO YA USAFIRISHAJI UMEME mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2019/02/tanzania-yashiriki-mkutano-wa-26-kuhusu.html

Subscribe to receive free email updates:

0 Response to "TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA 26 KUHUSU MIFUMO YA USAFIRISHAJI UMEME"

Post a Comment