Waitara awataka Wenyeviti na Madiwani kwenda na kasi ya JPM

Waitara awataka Wenyeviti na Madiwani kwenda na kasi ya JPM - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Waitara awataka Wenyeviti na Madiwani kwenda na kasi ya JPM, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Waitara awataka Wenyeviti na Madiwani kwenda na kasi ya JPM
kiungo : Waitara awataka Wenyeviti na Madiwani kwenda na kasi ya JPM

soma pia


Waitara awataka Wenyeviti na Madiwani kwenda na kasi ya JPM


NA HERI SHAABAN
Mwambawahabari
Madiwani na Wenyeviti wa Serikali ya Mtaa nchini watakiwa kusimamia majukumu yao ya kazi na kwenda na kasi ya Rais John Magufuli katika kuleta maendeleo.

Hayo yalisemwa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI )Mwita Waitara wakati wa mkutano wake na wananchi wa kata ya Kipunguni Jimbo la Ukonga Wilayani Ilala Dar es Salaam leo.

"Madiwani na Wenyeviti mmechaguliwa na wananchi kama wawakilishi nataka mlete maendeleo katika maeneo yenu nchini mwende na kasi ya JPM serikali ya awamu ya tano kila kiongozi anatakiwa kuwajibika " alisema Waitara

Waitara alisema kiongozi yoyote ambaye atashindwa kutimiza wajibu wake katika kutatua changamoto za wananchi katika serikali ya awamu ya tano hafai inatakiwa kuomba likizo kukaa pembeni kuwapisha wengine.

Alisema pia katika jambo la maendeleo  inatakiwa kuitisha vikao  kuwashirikisha wananchi  wao kupanga pamoja katika miradi wanayokubaliana.

Katika hatua nyingine Waitara amepiga marufuku michango kwa wanafunzi nchini   wa shule za msingi na Sekondari.


"Mimi kama mwakilishi wa Rais nimeelekezwa na bosi wangu Seleman Jaffo nisimamie elimu na mwenzangu atasimamia upande wa afya  hivyo marufuku michango kwa wanafunzi wapya wa darasa la kwanza na Kidato cha kwanza" alisema


Akielezea changamoto za Kata ya Kipunguni Jimbo la Ukonga alisema Barabara ya Diwani Bombambili ujenzi wake unatarajia kuanza hivi karibuni mpaka Nyeburu Wakala wa Barabara TARURA watajenga na fedha zilizotengwa Bilioni 6.

Kuhusu changamoto ya maji Kipunguni yanatarajia kufika wakati wowote  na suala huduma ya afya Serikali tayari imetenga shilingi milioni 700 kwa ajili ya hospitali  ya Wilaya eneo la Kivule.

Aidha pia alielezea mikopo ya asilimia 10 ya Wanawake,Vijana na Walemavu alisema wananchi wote itawafikia mikopo hiyo wale waliokamilisha taratibu za usajili na Watendaji watakaokwamisha zoezi hilo watachukuliwa hatua.




Hivyo makala Waitara awataka Wenyeviti na Madiwani kwenda na kasi ya JPM

yaani makala yote Waitara awataka Wenyeviti na Madiwani kwenda na kasi ya JPM Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Waitara awataka Wenyeviti na Madiwani kwenda na kasi ya JPM mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/11/waitara-awataka-wenyeviti-na-madiwani.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Waitara awataka Wenyeviti na Madiwani kwenda na kasi ya JPM"

Post a Comment