CHINA DASHENG BANK LIMITED YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM, KUSAIDIA UCHUMI WA VIWANDA

CHINA DASHENG BANK LIMITED YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM, KUSAIDIA UCHUMI WA VIWANDA - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa CHINA DASHENG BANK LIMITED YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM, KUSAIDIA UCHUMI WA VIWANDA, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : CHINA DASHENG BANK LIMITED YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM, KUSAIDIA UCHUMI WA VIWANDA
kiungo : CHINA DASHENG BANK LIMITED YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM, KUSAIDIA UCHUMI WA VIWANDA

soma pia


CHINA DASHENG BANK LIMITED YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM, KUSAIDIA UCHUMI WA VIWANDA

NA K-VIS BLOG

BENKI mpya ya China Dasheng Bank Limited, inaanza kutoa huduma leo Jumatatu Novemba 26, 2018, jijini Dar es Salaam, ikiwa na mtaji wa kuanzia wa dola za kimarekani milioni 40 sawa na shilingi za kitanzania bilioni 92, Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya benki hiyo Bw. Yu Jiaqin amesema.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa benki hiyo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam, Bw. Yu Jiaqin amesema benki hiyo ni benki ya kibiashara inayomilikiwa na makampuni sita ya serikali ya China yakishirikiana na makampuni binafsi kutoka mji wa Shanghai na Jiangsu.

Benki hii inalenga kutoa huduma kwa makampuni makubwa ya kichina yanayofanya miradi mbalimbali hapa nchini, lakini pia watanzania wanaofanya biashara na China ikizingatia makundi yote ya watu wenye kipato cha chini, cha kati na cha juu, alisema Bw. Jiaqin.

“Tutatoa huduma za bidhaa zote za kawaida za kibenki kama vile akaunti za akiba, akaunti za kudumu na za muda maalum, mikopo ya muda mfupi na muda mrefu na mikopo hii itatolewa kwa shilingi za kitanzania pamoja na fedha za kigeni.” Alibainisha Mwenyekiti huyo wa bodi.

Aidha Naibu Afisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo, Bi Nunu Saghaf alishukuru Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwa kutoa leseni ya kufanya biashara kwa benki yake na kuahidi kuisaidia serikali ya Tanzania katika kufikia malengo yake ya uchumi wa viwanda ifikapo mwaka 2025.
Balozi wa China nchini Tanzania Mhe.Wang Ke, (katikati), akiungana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, (wapili kushoto), Mwenyekiti wa Banki mpya ya China Dasheng Bank Limited, Yu Jiaqin, (wapili kulia), Afisa mwandamizi kutoka Banki Kuu ya Tanzania, Sadaat Mussa (wakwanza kulia) na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara kutoka China, Zhujin Feng, baada ya kukata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa benki hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Benki hiyo imeanza kutoa huduma leo Jumatatu Novemba 26, 2018 ikiwa na mtaji wa kuanzia wa dola za kimarekani milioni 40 sawa na shilingi za kitanzania bilioni 92, Mwenyekiti wa benki hiyo amesema.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda, akitoa hotuba yake.
Balozi wa China nchini Tanzania, Mhe. Wang Ke akitoa hotuba yake.
Naibu Afisa Mtendaji Mkuu wa China Dasheng Banki Limited, Bi. Nunu Saghaf (watatu kushoto mstari wa mbele akiwa na wageni mbalimbali kwenye hafla hiyo ya uzinduzi.
Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla hiyo.



Hivyo makala CHINA DASHENG BANK LIMITED YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM, KUSAIDIA UCHUMI WA VIWANDA

yaani makala yote CHINA DASHENG BANK LIMITED YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM, KUSAIDIA UCHUMI WA VIWANDA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala CHINA DASHENG BANK LIMITED YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM, KUSAIDIA UCHUMI WA VIWANDA mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/11/china-dasheng-bank-limited-yazinduliwa.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "CHINA DASHENG BANK LIMITED YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM, KUSAIDIA UCHUMI WA VIWANDA"

Post a Comment