title : NHC YAKABIDHI KITUO CHA POLISI KWA JESHI LA POLISI JIJINI DAR ES SALAAM
kiungo : NHC YAKABIDHI KITUO CHA POLISI KWA JESHI LA POLISI JIJINI DAR ES SALAAM
NHC YAKABIDHI KITUO CHA POLISI KWA JESHI LA POLISI JIJINI DAR ES SALAAM
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC) limekabidhi Kituo chá Polisi kwa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kilichojengwa kwa thamani ya zaidi ya sh.milioni 75 ili kiweze kutoa huduma kwa jamii inayozunguka eneo la Changanyikeni Kibada jijini Dar es Salaam.
Ujenzi wa kituo hicho kwa NHC sera ya utekelezaji wa huduma kwa jamii katika sehemu mbalimbali zilizokuwa na miradi na hata sehemu zingine ambapo miradi haifayiki..
Akizungumza kabla ya ufunguzi na makabidhiano, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Félix Maagi amesema kuwa kabla ya ujenzi wa nyumba 248 za shirika hilo katika eneo la Kibada, walipanga kujenga kituo hicho ambacho sasa kimesha kamilika ikiwa kuhakikisha wakazi wanaoishi katika nyumba hizo wanakuwa na ulinzi wao na mali zao.
Amesema kituo hicho chenye vyumba viwili vya mahabusu (wakiume na wakike), ofisi ya mkuu wa kituo, vyoo viwili vya maofisa na vya mahabusu.
"Kumekuwa na mawasiliano na Jeshi la Polisi kukifanyika kwa maboresho kabla ya kukikabidhi kwa kuhakikisha kituo kimekidhi viwango vya ubora vya mahitaji ya polisi na kitawahudumia wakazi wengi wa eneo hili, "amesema Maagi.
Naye Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Awadhi Haji, alilishukuru shirika hilo kwa kuonesha uzalendo na kueleza kuwa, usalama ni muhimu kwa wananchi ili waweze kuishi kwa amani na kujiletea maendeleo.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Awadhi Haji akizungumza katika halfa ya makabidhiano ya kituo cha polisi Kibada kilichojengwa na Shirika la Taifa la Nyumba (NHC) jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Félix Maagi akizungumza kuhusiana na ujenzi wa kituo cha polisi ikiwa ni sera ya shirika hilo katika hafla makadhibiano ya kituo polisi yaliyofanyika Kibada jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Changanyikeni, Gwalugano Mwakatobe akieleza umuhimu wa kujengwa kwa kituo cha polisi katika eneo lake katika hafla ya makabidhiano ya kituo cha polisiliyofanyika kibada jijini Dar es Salaam.
.Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Awadh Haji akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kituo cha Polisi
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Awadh Haji akiwa katika picha ya pamoja na wananchi wa Kibada na . Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Félix Maagi
Hivyo makala NHC YAKABIDHI KITUO CHA POLISI KWA JESHI LA POLISI JIJINI DAR ES SALAAM
yaani makala yote NHC YAKABIDHI KITUO CHA POLISI KWA JESHI LA POLISI JIJINI DAR ES SALAAM Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala NHC YAKABIDHI KITUO CHA POLISI KWA JESHI LA POLISI JIJINI DAR ES SALAAM mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/10/nhc-yakabidhi-kituo-cha-polisi-kwa.html
0 Response to "NHC YAKABIDHI KITUO CHA POLISI KWA JESHI LA POLISI JIJINI DAR ES SALAAM"
Post a Comment