CWT Kilolo chawazawadia bati walimu wastaafu

CWT Kilolo chawazawadia bati walimu wastaafu - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa CWT Kilolo chawazawadia bati walimu wastaafu, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : CWT Kilolo chawazawadia bati walimu wastaafu
kiungo : CWT Kilolo chawazawadia bati walimu wastaafu

soma pia


CWT Kilolo chawazawadia bati walimu wastaafu

CHAMA  cha  walimu   Tanzania (CWT)  wilaya ya  Kilolo  mkoani Iringa  kimetoa  bati   500  zenye  thamani  ya  zaidi ya  shilingi milioni 8.5 kwa   mwalimu  mstaafu  25  kama  sehemu ya  kuwaaga na  kuwapongeza kwa  utumishi  bora katika  kazi  hiyo ya  ualimu .

Akikabidhi   bati  hizo jana  wakati wa  hafla  fupi ya  kuwaaga  walimu  hao  mgeni  rasmi katika  hafla  hiyo afisa   utumishi  wa  Halmashauri ya  wilaya ya  Kilolo   Josephat  Kayombo   pamoja na  kupongeza   CWT wilaya ya   Kilolo  kwa  kutambua  mchango  wa   walimu   wenzao  ambao  wamestaafu  bado  alitoa  wito  kwa  walimu   waliopo kazini  kuendelea kujituma  kufanya kazi hiyo na  kujiepusha  na  utovu  wa  nidhamu .

Kayombo  alisema   serikali  imeendelea  kuwajali  watumishi  wote  wa umma  wakiwemo  walimu na kuendelea  kulipa  stahiki  zao ambazo  wamekuwa  wakizidai hivyo  ni lazima  kwa  watumishi hao kutimiza  majukumu yao  kwa  ufanisi na  kuepuka   kuonyesha  utovu wa  nidhamu  na  jeuri  pale  mwajili  ambapo amua  kumpangia kituo kipya  cha kazi .

"  Walimu  ni  kielelezo  tosha  kwa  jamii na hakuna yeyote  anayeweza  kujisifu  kwa  mafanikio yake  bila  kutambua  mchango wa  mwalimu   hivyo ni vema  walimu  kwa  umuhumu  wenu  huo kuendelea   kulenda   heshima  yenu kwa   kuonyesha  nidhamu na  kuzingatia  kanuni  na  taratibu za  kazi  na  kujiepusha  kuwa  na  nidhamu  mbovu "  alisema  Kayombo 

 Pia  alisema    kwa  kuwa  serikali  imeendelea  kuwalipa  mafao  yao   wastaafu    ni  vema  walimu    wastaafu  kuwa makini na  wimbi la  matapeli  ambao  wamekuwa  wakizunguka katika vijiji mbali mbali  vya  wilaya ya  Kilolo  na  kuorodhesha majina ya  walimu  wastaafu  kwa  lengo la  kuwatapeli   mafao  yao  ya  ustaafu .

Alisema  kuwa  kiasi cha  fedha  ambacho  wanakipata  baada ya  kustaafu  kinaweza  kuja  kuwa msaada  mkubwa  kwao mbele ya  safari    hivyo  umakini unahitajika  kwa  kuwaepuka  matapeli  hao .

Aidha  Kayombo  aliwapongeza  walimu  wastaafu  wa  wilaya ya  Kilolo kwa  kustaafu kwa  heshima na  kuwa katika  zoezi la kuhakiki watumishi   wenye vyeti  feki  walimu hao walihakikiwa  na hadi  wanastaafu   hakukuwa na mwalimu hata  mmoja  aliyekutwa na  cheti  feki .

Kuhusu  uhamisho  wa  walimu uliofanyika  alisema  kuwa anasikitishwa na  baadhi ya  walimu  kuonyesha  kugoma  kuripoti katika  kituo  alichopangiwa  na  hadi  sasa  baadhi yao  hawajaripoti  popote  jambo ambalo  wameanza  kuwafuatilia  walimu hao .

"  Kulikuwa  na uhamisho wa aina  mbili  walimu   kutoka  sekondari  kwenda  shule za msingi  na  walimu wa  shule za  msingi   na yalitolewa  maelezo  kuwa  walimu  wa  shule za msingi  wamepungua na  sekondari  kuna  walimu wa masomo ya sanaa  ambao  walikuwa  wamezidi  na hawakuwa na kazi yoyote    ndipo  ilitolewa amri  kuwatoa  huko na  kwenda  kufundisha  shule za  msingi hapo  ndipo  ilipoleta  shida  na  kuwa  walimu  wote wamelipwa  kila  mmoja zaidi ya  shilingi 500,000 kwa  walimu  wote zaidi ya 90 "  alisema  Kayombo 

Kuwa  ila  bado  watu  wanakataa  kwenda  kuripoti kituoni  hivyo  aliwataka  walimu hao  kwenda kazini  huku  malipo  mengine   wakiendelea  kulipwa  kwa  awamu na  Halmashauri ya  Kilolo  imeendelea  kuwalipa  walimu hao .
Afisa utumishi  wilaya ya  Kilolo  mkoani Iringa Joseptah kayombo (kulia)  akiwa na  viongozi wa chama cha walimu Tanzania (CWT)  wilaya ya  Kilolo wakiwakabidhi bati  walimu  wastaafu 25  kila  mmoja bati 20.
 Viongozi wa CWT  Kilolo (kulia)  wakiwakabidhi walimu wastaafu 25 zawadi ya bati 20 kila  mmoja .

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


Hivyo makala CWT Kilolo chawazawadia bati walimu wastaafu

yaani makala yote CWT Kilolo chawazawadia bati walimu wastaafu Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala CWT Kilolo chawazawadia bati walimu wastaafu mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/10/cwt-kilolo-chawazawadia-bati-walimu.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "CWT Kilolo chawazawadia bati walimu wastaafu"

Post a Comment