title : WAGOMBEA SIMBA KUCHUNGUZWA.
kiungo : WAGOMBEA SIMBA KUCHUNGUZWA.
WAGOMBEA SIMBA KUCHUNGUZWA.
Kamati ya Uchaguzi ya Simba, leo Jumapili inatarajiwa kuzipitia fomu za wagombea wa nafasi za uongozi ndani ya klabu hiyo baada ya leo kuhitimisha zoezi la upokeaji fomu.Simba inatarajiwa kufanya uchaguzi mkuu Novemba 3, mwaka huu kwa kuchagua viongozi wa nafasi za mwenyekiti na wajumbe. Zoezi hilo lilionekana kusuasua kutokana na kigezo cha mgombea kuwa na elimu ya kiwango cha digrii kuwashinda wengi hali iliyosababisha kuwa na wagombea wawili tu wa nafasi ya uenyekiti ambao ni Sued Nkwabi na Mtemi Ramadhani na wajumbe 19.
Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi Simba, Boniface Lihamwike alisema kuwa, hakuna muda wa kupoteza kwa sasa kwa kuwa utaratibu upo wazi kama ambavyo hawakuongeza siku za kuchukua fomu ndivyo itakavyokuwa wakati wa kurudisha fomu.
“Tulitoa siku tano kwa ajili ya kukamilisha zoezi la ujazaji wa fomu ambapo mwisho wake ni Jumamosi ambayo ni tarehe 15 (jana) hivyo wale wote waliochukua fomu wanapaswa warejeshe ili tuweze kuendelea na mchakato wa uchaguzi kwa mujibu wa sheria.
“Siku tatu zitakuwa maalumu kwa ajili ya kuzipitia fomu na muda mwafaka kwa ajili ya kuweza kutazama wale wenye pingamizi na watakaokata rufaa baada ya kumaliza hatua hiyo kitakachofuata ni kutangaza wale ambao wamekidhi vigezo na masharti,” alisema Lihamwike
Hivyo makala WAGOMBEA SIMBA KUCHUNGUZWA.
yaani makala yote WAGOMBEA SIMBA KUCHUNGUZWA. Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala WAGOMBEA SIMBA KUCHUNGUZWA. mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/09/wagombea-simba-kuchunguzwa.html
0 Response to "WAGOMBEA SIMBA KUCHUNGUZWA."
Post a Comment