TPA KUHUDUMIA TANI MILIONI I4

TPA KUHUDUMIA TANI MILIONI I4 - Hallo rafiki WORLD MAELEZO LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa TPA KUHUDUMIA TANI MILIONI I4, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala biashara, makala general, makala hobby, makala karibuni info, makala michezo, makala siasa, makala utamaduni, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : TPA KUHUDUMIA TANI MILIONI I4
kiungo : TPA KUHUDUMIA TANI MILIONI I4

soma pia


TPA KUHUDUMIA TANI MILIONI I4


Mamlaka  ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) inatarajia kuhudumia tani 14,374,400 yakiwemo makontena (TEUs) 208,000 katika vitengo vinavyoendeshwa na mamlaka hiyo kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2018/2019.
Kitengo cha Kontena katika Bandari ya Dar es Salaam (TICTS) pia kinatarajia kuhudumia makontena (TEUs) 489,300 katika mwaka huo wa fedha.
Mkurugenzi Mkuu wa (TPA), Deusdedit Kakoko amesema hayo Dar es Salaam wakati akielezea mpango na bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019 ya mamlaka hiyo.
"Tunatarajia kukusanya mapato ya jumla ya Sh bilioni 1,012.586, matumizi ni Sh bilioni 778.297 na kupata ziada ya Sh bilioni 234.289," amesema.
Pia alisema wanatarajia kuhudumia meli 2,736 zenye ukubwa wa (GRT) milioni 35.880 na kati ya hizo meli 1,307 ni za Kimataifa (Deep Sea), meli 786 ni za mwambao na meli 670 zitahudumiwa katika bandari za Maziwa.
Kakoko alisema, wataimarisha mfumo na kuongeza matumizi ya Tehama kwa malipo kwa kutumia mtandao (e-payment) na kukamilisha mradi na kutumia mfumo mpya wa 'Enterprise Resource Planning'(ERP) katika kutoa huduma na ukusanyaji wa mapato.
Aidha amesema watakusanya mapato kwa wakati na kuziba mianya yote ya upotevu wa mapato na kukusanya kwa kupitia benki sambamba na kuzingatia matumizi ya 'flow meters' na skana katika kuhakikisha shehena ya mafuta na shehena kwenye kontena.
"Tumejiwekea mikakati ya kuvutia shehena kwa kuboresha huduma za mamlaka kwa kutekeleza miradi mbalimbali kwa wakati uliopangwa sambamba na kuimarisha ulinzi na usalama katika bandari za Mamlaka," amesema. 


Hivyo makala TPA KUHUDUMIA TANI MILIONI I4

yaani makala yote TPA KUHUDUMIA TANI MILIONI I4 Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala TPA KUHUDUMIA TANI MILIONI I4 mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/08/tpa-kuhudumia-tani-milioni-i4.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "TPA KUHUDUMIA TANI MILIONI I4"

Post a Comment