title : MKUU MPYA WA WILAYA YA BAGAMOYO ZAINABU KAWAWA AFUNGUA RASMI MAFUNZO YA AWALI YA JESHI LA AKIBA KWA VIJANA 183 CHALINZE
kiungo : MKUU MPYA WA WILAYA YA BAGAMOYO ZAINABU KAWAWA AFUNGUA RASMI MAFUNZO YA AWALI YA JESHI LA AKIBA KWA VIJANA 183 CHALINZE
MKUU MPYA WA WILAYA YA BAGAMOYO ZAINABU KAWAWA AFUNGUA RASMI MAFUNZO YA AWALI YA JESHI LA AKIBA KWA VIJANA 183 CHALINZE
VICTOR MASANGU, CHALINZE
MKUU mpya wa Wilaya ya Bagamoyo Zainabu Kawawa amewataka vijana ambao wanahitimu mafunzo ya jeshi la akiba kuhakikisha wanakuwa wazalendo na nchi yao na kuachana kabisa na vitendo vya kujiingiza katika matukio ya kihalifu na badala yake wahakikishe wanazingatia sheria na taratibu zote zilizowekwa kwa lengo la kuweza kulinda hali ya ulinzi na usalama wa wananchi na mali zao.
Kauli hiyo aliitoa wakati wa sherehe za ufunguzi rasmi wa mafunzo ya awali ya jeshi la akiba ambayo yamefanyika katika kata ya Bwilingu na kuwajumusiha vipana wapatao 183 kutoka katika halmashauri ya Chalinze Wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani.
Mkuu huyo pia aliwahimiza vijana hao kuhakikisha wanakuwa na nidhamu ya hali ya juu katika kipindi chote cha mafunzo hayo ya kijeshi na kuzingatia maelekezo ambayo wanapatiwa na walimu wao kwa lengo la kuweza kujifunza mbinu mbali mbali ambazo zitaweza kuwa ni mkombozi mkubwa katika kulilinda Taifa la Tanzania na kuweza kukabiliana na wimbi la matukio ya uhalifu.
“Napenda kuchukua fursa hii kuwapongeza vijana ambao mmeweza kujitokeza katika mafunzo haya ya jeshi la akiba,lakini kitu kikukbwa ninawaomba muwe wazalendo na nchi yenu kwa kuhakikisha mnazingatia sheria na taratibu za nchi ikiwa ni sambamba na kuyatumia vizuri mafunzo mliyopatiwa kwa maslahi ya nchi na sio vinginevyo,”alisema
Mkuu mpya wa Wilaya ya Bagamoyo Zainabu Rashid Kawawa kulia akiwa na Mshauri wa jeshi la akiba wilayani humo wa kushoto Maj Chinguku wakati wa sherehe za ufunguzi rasmi wa mafunzo wa jeshi la akiba kwa vijana wapatao 183 ambayo yamefanyika katika kata ya Bwilingu halmashauri ya Chalinze.
Mkuu mpya wa Wilaya ya Bagamoyo Zainabu Kawawa wa kati kati akirukaruka mara baada ya kufungua mafunzo rasmi ya jeshi la akiba kwa vijana wapatao 183 hawapo pichani kutoka kata ya Bwilingu katika halmashauri ya Chalinze pembeni yake kulia ni Mshauri wa jeshi la akiba Wilayani Bagamoyo Maj Chinguku.
Mkuu mpya wa Wilaya ya Bagamoyo Zainabu Kawawa wa kati kati akirukaruka mara baada ya kufungua mafunzo rasmi ya jeshi la akiba kwa vijana wapatao 183 hawapo pichani kutoka kata ya Bwilingu katika halmashauri ya Chalinze pembeni yake kulia ni Mshauri wa jeshi la akiba Wilayani Bagamoyo Maj Chinguku.
Hivyo makala MKUU MPYA WA WILAYA YA BAGAMOYO ZAINABU KAWAWA AFUNGUA RASMI MAFUNZO YA AWALI YA JESHI LA AKIBA KWA VIJANA 183 CHALINZE
yaani makala yote MKUU MPYA WA WILAYA YA BAGAMOYO ZAINABU KAWAWA AFUNGUA RASMI MAFUNZO YA AWALI YA JESHI LA AKIBA KWA VIJANA 183 CHALINZE Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala MKUU MPYA WA WILAYA YA BAGAMOYO ZAINABU KAWAWA AFUNGUA RASMI MAFUNZO YA AWALI YA JESHI LA AKIBA KWA VIJANA 183 CHALINZE mahali kiungo https://wordmaelezo.blogspot.com/2018/08/mkuu-mpya-wa-wilaya-ya-bagamoyo-zainabu.html
0 Response to "MKUU MPYA WA WILAYA YA BAGAMOYO ZAINABU KAWAWA AFUNGUA RASMI MAFUNZO YA AWALI YA JESHI LA AKIBA KWA VIJANA 183 CHALINZE"
Post a Comment